Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 12 Sitting 7 Water and Irrigation Wizara ya Maji 111 2023-09-06

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: aliuliza: -

Je, lini Serikali itapeleka maji safi na salama katika Kata ya Kwekanga?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shabani Omari Shekilindi, Mbunge wa Jimbo la Lushoto, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua adha ya maji wanayoipata wakazi wa Kata ya Kwekanga yenye Vijiji vitano vya Kwekanga, Mziragembei, Bombo-Kamghoboro, Mategho na Mshangai. Katika kukabiliana na changamoto hiyo, Serikali katika Mwaka wa fedha 2023/2024, itafanya utafiti wa maji chini ya ardhi (Hydrogeological survey) pamoja na kuchimba visima virefu katika Kata za Kwekanga, Kwai, Kilole, Malindi, Makanya na Lushoto Mjini. Kazi hiyo inatarajiwa kufanyika na kukamilika mwezi Disemba, 2023. Uendelezaji wa visima hivyo utafanyika mara baada ya uchimbaji kukamilika na maji kupatikana.