Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: aliuliza: - Je, lini Serikali itapeleka maji safi na salama katika Kata ya Kwekanga?

Supplementary Question 1

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na namshukuru Waziri kwa majibu mazuri. Changamoto ya kukosa maji katika Kata ya Kwekanga, Kwai, Malibwi, Mbwei, Makanya na Mlola ni changamoto muda mrefu sana. Suala hili nimeliongelea zaidi ya takribani Mikutano Kumi bila mafanikio yoyote na wananchi wangu wakiendelea kupata tabu ya maji.

Je, nini mkakati wa dharura wa Serikali kupeleka gari la kuchimba visima katika kata nilizozitaja?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kuna Mradi wa Magamba eneo la Gelwa Ali unaitwa Mtaa Na. 9 na survey imeshafanyika. Mradi ule ukikamilika unakwenda kuhudumia kata zaidi 13. Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya kutekeleza mradi huo?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote napenda kumpongeza Mheshimiwa Shekilindi, amekuwa mfuatiliaji nilikuahidi nitafika jimboni Mheshimiwa Mbunge, kipindi kilichopita sikuweza, baada ya Bunge hili nitahakikisha tunakwenda kuona maeneo haya na kuweka msisitizo ili kuhakikisha miradi hii inatekelezeka.

Mheshimiwa Naibu Spika, mkakati wa dharura tayari Mheshimiwa Mbunge tumekutengea shilingi milioni 300. Tunataka baada ya ukamilishaji wa hii survey visima hivi vichimbwe na hatutaishia tu kuchimba visima. Tutahakikisha tunasambaza na kujenga vichotea maji kwa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili, fedha za Miradi ya Mbao tayari usanifu umekamilika. Mheshimiwa Mbunge, tayari tutaendelea kukuletea fedha. Sasa hivi tumekutengea milioni 300 na mgao ujao tutahakikisha tunakutengea fedha. Mimi mwenyewe nitakuja jimboni kuleta msukumo hii miradi iweze kutekelezeka.