Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 4 Sitting 2 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 30 2016-09-07

Name

Khamis Mtumwa Ali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiwengwa

Primary Question

MHE. KHAMIS M. ALI aliuliza:-
Kwa muda mrefu sasa baadhi ya wakuu wa Vituo vya polisi hasa Zanzibar hutumia pesa ao za mishahara kulipa huduma za umeme katika vituo hivyo;
Je, Serikali ina utaratibu gani wa kuwalipa au kuwarejeshea pesa wanazotumia kulipa umeme katika vituo hivyo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Khamisi Mtumwa Ali Mbunge wa Kiwengwa kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikirejesha fedha hizo za umeme endapo askari amelipia au amenunua umeme kwa ajili ya kituo cha polisi kwa kupitia utaratibu wa kujaza fomu za madai na kuambatisha risiti ya malipo hayo kisha kuziwasilisha kwa mhasibu kwa ajili ya malipo yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo Wizara yangu imekuwa ikijitahidi kupeleka fedha za kulipia umeme kwa wakati ili kuondoa usumbufu unaojitokeza kwa askari walioko vituoni na makambini kadri ya hali ya uwezo utakapokuwa unaruhusu.