Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 36 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 466 2023-05-30

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Primary Question

MHE. JERRY W. SILAA aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Pugu - Majohe - Viwege njia nne na Kampala - Bwera - Rada hadi Chuo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Jerry William Silaa, Mbunge wa Jimbo la Ukonga, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikizifanyia matengenezo barabara za Jimbo la Ukonga zikiwemo barabara za njia nne Pugu – Majohe hadi Viwege na Kampala – Bwera – Rada hadi Chuo ambapo katika Mwaka wa Fedha 2022/2023 jumla ya shilingi milioni 701.67 zimetengwa kwa ajili ya matengenezo yenye urefu wa kilomita 20.7 na kazi zinaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ongezeko la matumizi katika barabara hizo limesababisha matengenezo yanayofanyika kutokudumu kwa muda mrefu. Hivyo Serikali imeingiza barabara hizi katika mpango wa uendelezaji wa Jiji la Dar es Salaam (DMDP) awamu ya pili, ili barabara hizo zijengwe kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa mradi upo katika hatua za awali za kufanya usanifu.