Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 36 Water and Irrigation Wizara ya Maji 476 2023-05-30

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatoa bei moja elekezi kwa kila unit moja ya maji Wilayani ya Karatu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Daniel Awack Tlemai, Mbunge wa Jimbo la Karatu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, huduma ya majisafi na usafi wa mazingira mjini Karatu inatolewa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Karatu (Karatu Urban Water Supply and Sanitation Authority - KARUWASA). Awali kulikuwa na changamoto ya kuwepo kwa Taasisi mbili zinazotoa huduma ya maji ambazo ni Karatu Village Water Supply (KAVIWASU) na KARUWASA na kila moja ilikuwa na bei yake. Mwezi Agosti 2022, Serikali iliziunganisha taasisi hizo na kuwa na taasisi moja inayoitwa KARUWASA na kutoa bei elekezi ya maji ya shilingi 1,300 kwa unit moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa eneo la Karatu Vijijini linalohudumiwa na RUWASA, Serikali ilitoa bei elekezi kulingana na teknolojia inayotumika kuwafikishia wananchi maji na bei hizo zinafuatwa.