Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatoa bei moja elekezi kwa kila unit moja ya maji Wilayani ya Karatu?

Supplementary Question 1

MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu ya Serikali nina swali moja la nyongeza. Kama katika Mji wa Karatu waliweza kushusha bei kutoka shilingi 3,500 mpaka shilingi 1,300 kwa unit. Je, inashindikana nini katika jimbo hilo hilo katika eneo la RUWASA vijijini majini kuuzwa kwa shilingi 2,500, kwa nini kwenye jimbo moja isishushwe bei ikawa ya uwiano Karatu Mjini na Karatu Vijijini ikawa na bei moja kuliko kuwa na bei mbili katika Mji wa Karatu? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Daniel Awack Tlemai, Mbunge wa Karatu kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, bei za maji hazifanani kwa sababu ya teknolojia zinazotumika kusambaza maji. Teknolojia ambayo inatumika eneo la RUWASA ni tofauti na pale mjini. Kwa hiyo sisi kama Wizara tunachokifanya ni kuhakikisha bei zinakuwa rafiki kwa wananchi wa eneo husika. Kwa hiyo, kwenye maeneo haya ambayo yanahudumiwa na RUWASA bei ziko tofauti kwa namna ambavyo maji yanasukumwa na gharama za uendeshaji.