Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 36 Energy and Minerals Wizara ya Madini 478 2023-05-30

Name

Kabula Enock Shitobela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KABULA E. SHITOBELA aliuliza:-

Je, Serikali haina njia mbadala ya matumizi ya matimba kama ngazi ambayo yanamaliza miti na hivyo kuharibu mazingira?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

WAZIRI WA MADINI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kabula Enock Shitobela, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuwa magogo ya miti ni moja ya teknolojia rahisi na muhimu katika ujenzi wa migodi ya chini ya ardhi kwenye shughuli za uchimbaji mdogo wa madini nchini, ambapo miti hiyo hutumika katika ujenzi wa kuta na dari za migodi ili kuweka mazingira salama ya migodi midogo kwa wachimbaji. Wachimbaji wadogo hununua miti hiyo kutoka kwenye hifadhi za misitu na mashamba ya miti kupitia mawakala wa miti kwa kufuata taratibu za uvunaji wa miti. Teknolojia ya matumizi ya magogo ya miti imeenea zaidi kwa wachimbaji wadogo kwa kuwa inasaidia kuimarisha usalama wa migodi na haihitaji uwekezaji mkubwa wakati wa ujenzi wa migodi hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia zipo teknolojia nyingine zinazotumika kwenye ujenzi wa migodi ya chini ya ardhi ambazo hutumia zege na vyuma ili kuimarisha kuta na dari za migodi hiyo. Teknolojia ya zege na vyuma hutumiwa zaidi na Wachimbaji wa Kati na Wakubwa kwa sababu ni ghali ukilinganisha na wachimbaji wadogo.