Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 39 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 502 2023-06-02

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza:-

Je, lini Sheria italetwa kupunguza michakato ya utangazaji wa Miradi ya TARURA na fedha kusimamiwa na Mameneja wa Wilaya?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kassim Iddi Iddi, Mbunge wa Jimbo la Msalala, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Ununuzi wa Umma imetungwa ili kuweka uwiano mzuri wa haki na ushindani katika Ununuzi wa Umma na hutumika kwa Taasisi zote za Serikali na siyo TARURA pekee. Kwa mujibu wa muundo wa TARURA, fedha zote za miradi na utekelezaji wake umekasimiwa kwa Mameneja wa Wilaya. Malipo yote huandaliwa na Meneja wa Wilaya na kutumwa kwa Meneja wa Mkoa kwa ajili ya uidhinishwaji na ulipwaji kupitia mfumo wa Malipo Serikalini (MUSE). Aidha, Ofisi ya Mkoa kwa kushirikiana na Ofisi ya Meneja wa Wilaya, itaendelea kufanya tathmini kuhakikisha miradi inafanyika kwa kuzingatia thamani ya fedha ili iweze kukidhi uhitaji wake.