Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 41 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 531 2023-06-06

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga Jengo la OPD katika Kituo cha Afya cha Kintinku ambacho kimeanza kutumika bila kuwa na jengo hilo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya, Mbunge wa Jimbo la Manyoni Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha wa 2017/2018 Serikali ilitenga shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa Kituo cha Afya Kintinku. Aidha, majengo matano yalijengwa ikiwa ni pamoja na jengo la Wazazi, jengo la Upasuaji, jengo la Kufulia, jengo la kuhifadhia maiti na nyumba ya mtumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni imetenga shilingi milioni 20 katika mwaka wa fedha wa 2023/2024 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa jengo la OPD.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu msingi katika vituo vya afya kote nchini kikiwemo Kituo cha Afya Kintiku.