Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Jengo la OPD katika Kituo cha Afya cha Kintinku ambacho kimeanza kutumika bila kuwa na jengo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali kwanza nitumie fursa hii kuipongeza Serikali na kuishukuru wametupatia bilioni moja kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa shule ya sekondari ya wasichana ya Mkoa. Ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Afya cha Kintiku kinahudumia takribani Halmashauri tatu, Halmashauri ya Bahi, Halmashauri ya Chemba na baadhi ya vijiji vya Halmashauri ya Manyoni. Kituo hiki kipo kwenye high way ya kutoka Dodoma kwenda Mwanza. Je, lini Serikali itapeleka gari la wagonjwa (ambulance) ili iweze kusaidia kwenye kituo hicho?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili katika Kata ya Nkonko kuna kituo cha afya ambacho kilijengwa, vilevile walijenga jengo la x-ray ambalo bado halijakamilika. Je, lini Serikali itakamilisha jengo hilo la x-ray katika Kituo cha Afya cha Nkonko ili kiweze kuanza kutoa huduma? ahsante sana. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Pius Stephen Chaya, kwanza kuhusu hichi Kituo cha Afya cha Kintiku. Ni kweli ninakiri kwamba kituo hiki cha afya ni muhimu sana kwa sababu kipo barabarani na kama alivyosema Mheshimiwa Chaya ni kituo kinachohudumia Wilaya ya Chemba, kinachohudumia wakazi wa Wilaya ya Bahi na Wilaya ya Manyoni yenyewe na kipo kilometa takribani kama 26 ama 27 kutoka mpakani mwa Dodoma na Mkoa wa Singida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali hivi sasa imetenge bilioni 93 kwa ajili ya ununuzi wa magari 316 ya wagonjwa nchi nzima na kwa kuanzia kila Halmashauri itapata walau magari mawili ya wagonjwa. Tayari magari 117 yameshanunuliwa mpaka kufika mwezi Mei mwaka huu na tutahakikisha tunaweka kipaumbele kwenye vituo vya afya vya maeneo ya kimkakati kama Kituo cha Afya cha Kintiku.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili la Kituo cha Afya Kata ya Nkonko ambacho kinahitaji jengo la x-ray. Tutaangalia katika mwaka wa fedha 2023/2024 kuona ni namna gani Serikali Kuu itaongeza nguvu kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni kuweza kukamilisha ujenzi wa jengo hili la x-ray katika Kituo cha Afya cha Nkonko ili wananchi wa maeneo haya waweze kuanza kupata huduma za x-ray.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Jengo la OPD katika Kituo cha Afya cha Kintinku ambacho kimeanza kutumika bila kuwa na jengo hilo?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Kituo cha Afya Kiloleni Wilaya ya Busega hakina wodi za kulaza wagonjwa kabisa. Je, lini Serikali itajenga wodi hizo?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa ujenzi wa wodi ni katika vipaumbele vya Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Daktari Samia Suluhu Hassan, ujenzi wa wodi za kulaza wagonjwa, ujenzi wa vyumba vya upasuaji, ujenzi wa mochwari na kadhalika katika vituo vya afya na tutaangalia ni namna gani katika kituo cha afya alichokijata Mheshimiwa Midimu kinaweza kipata fedha kwa ajili ya ujenzi wa wodi hizi kule Wilayani Busega.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Jengo la OPD katika Kituo cha Afya cha Kintinku ambacho kimeanza kutumika bila kuwa na jengo hilo?

Supplementary Question 3

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kata ya Lahoda, Kata ya Jangalo na Kata ya Kinyamshindo zote zipo mpakani mwa Singida pia na Manyara. Je, ni lini mkakati wa Serikali wa kujenga vituo vya afya katika Kata hizo? ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Kata hii ya Lahoda, Jangalo na nyinginezo zilizokuwepo pembezoni katika Halmashauri ya Wilaya ya Chemba, Serikali itaweka kipaumbele kuhakikisha kwamba tunaanza ujenzi wa majengo ambayo yanahitajika kwenye vituo hivi vya afya na tutaangalia katika bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 ni kiasi gani kimetengwa kwa ajili ya Halmashauri ya Wilaya ya Chemba ili tuweze kupeleka fedha hizi kuanza ujenzi wa vituo hivi vya afya.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Jengo la OPD katika Kituo cha Afya cha Kintinku ambacho kimeanza kutumika bila kuwa na jengo hilo?

Supplementary Question 4

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na mimi niulize swali dogo la nyongeza.

Wananchi walihamasika sana katika ujenzi wa vituo vya afya pamoja na zahanati. Je, Serikali hamuoni kwamba kuna haja ya kumaliza yale maboma yote nchi nzima kabla hamjaanza ujenzi mpya?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nimfahamishe Mheshimiwa Bulaya kwamba Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Mama Samia Suluhu Hassan ilianza ujenzi wa vituo vya afya 234 nchi nzima ambavyo vimekamilika na ilitumika gharama ya bilioni 117. Sasa tunaangalia kutafuta fedha kwa ajili ya ku-support jitihada za wananchi katika maeneo mbalimbali nchini, kwa ajili ya umaliziaji wa vituo vya afya na zahanati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimalizie tu kwa kusema kuna shilingi milioni 50 ambazo zilipelekwa katika kila Halmashauri kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa zahanati za maeneo ambayo wananchi walianza ujenzi wenyewe. Hii inaonesha ni namna gani Serikali hii ya Daktari Samia Suluhu Hassan ipo committed katika ku-support jitihada za wananchi ambazo wameanza kujipelekea maendeleo.