Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 41 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 532 2023-06-06

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga Vituo vya Afya katika Kata ya Kwai na Makanya Lushoto?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shabani Omari Shekilindi, Mbunge wa Jimbo la Lushoto, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 Serikali ilitenga shilingi bilioni 117 kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vya Afya 234 kwenye Kata za kimkakati ikiwemo Halmashauri ya Wilaya ya Lushoto ambayo iliyotengewa shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Lunguza HC.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya kuboresha miundombinu ngazi ya Afya ya Msingi ikiwa ni pamoja na ujenzi wa vituo vya afya kwenye Kata za kimkakati kote nchini zikiwemo Kata za Kwai na Makanya.