Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Vituo vya Afya katika Kata ya Kwai na Makanya Lushoto?

Supplementary Question 1

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni muda mrefu sasa Kituo cha Afya Mlola hakina gari la wagonjwa na hii imepelekea hasa kwa wagonjwa mahtuti kupelekwa na bodaboda katika Hospitali ya Wilaya ya Lushoto. Je, Serikali lini itapeleka gari la wagonjwa katika Kituo cha Afya Mlola ili kuokoa maisha ya wananchi wetu?

Swali la pili, nimeongea kwa muda mrefu sana kuhusu kupeleka fedha katika Kituo cha Afya Gare lakini mpaka sasa hivi hakuna mafanikio yoyote, kama waswahili wanavyosema kuona ni kuamini. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri upo tayari kuongozana na mimi kwenda kuona nguvu za wananchi wale wa Gare kwa ajili ya ku-support Kituo kile cha Afya Gare?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya Mheshimiwa Shekilindi kwanza nianze kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa sababu amekua akifuatilia sana suala hili la magari katika Kituo cha Afya Mlola.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye kumjibu maswali yake mawili ya nyongeza hili la magari Serikali hii ya Awamu ya Sita ya Daktari Samia Suluhu Hassan imetenga fedha shilingi bilioni 93 kwa ajili ya ununuzi wa magari 316 ambayo kila Halmashauri ya Wilaya itapata walau magari mawili ya kubebea wagonjwa. Vilevile kuna bilioni 61 ambayo Serikali hii ya Daktari Samia Suluhu Hassan imetenga kwa ajili ya ununuzi wa magari mengine ambayo kila Halmashauri itapata gari moja walau la supervision katika Halmashauri za Wilaya ili wataalam wetu wa afya waweze kutembelea zahanati zetu na vituo vyetu vya afya. Hivyo nimhakikishie Mheshimiwa Shekilindi kwamba tutahakikisha vilevile katika magari haya mgao huo basi Mlola nayo inapewa kipaumbele kupata gari hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili la Kituo cha Afya cha Gare kule Wilayani Lushoto nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge niko tayari kuongozana naye Mheshimiwa Shekilindi, kuelekea Wilayani Lushoto kwa ajili ya kuweza kukagua jitihada hizi za wananchi na kuona ni namna gani Serikali kuu inaweza ika-support juhudi hizi za wananchi wa eneo la Gare.

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Vituo vya Afya katika Kata ya Kwai na Makanya Lushoto?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi na mimi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Je, lini Serikali itatekeleza ahadi ya Rais wa Awamu ya Tano ya kujenga Kituo cha Afya katika Kata ya Mulungu Jimboni Muhambwe?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la nyongeza la Daktari Samizi la lini Serikali itatekeleza ahadi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kujenga kituo cha afya. Tutaangalia ahadi hii na nitakaa na Mheshimiwa Samizi kuona ni namna gani tunaweza tukakaa na wataalam wetu kuona tunapataje fedha za kutekeleza ahadi hii katika mwaka wa fedha wa 2023/2024. (Makofi)