Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 41 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 533 2023-06-06

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA K.n.y. MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza:-

Je, lini Shule ya Sekondari Kayuki itafanyiwa ukarabati kama alivyoagiza Mheshimiwa Waziri Mkuu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Anton Albert Mwantona, Mbunge wa Jimbo la Rungwe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, taratibu za kutekeleza agizo lililotolewa na Mheshimiwa Waziri Mkuu la kukarabati Shule ya Sekondari Kayuki zinaendelea ambapo Halmashauri imekamilisha BOQ kwa ajili ya ukarabati wa Shule ya Sekondari Kayuki na imebainika kuwa shilingi milioni 776 zinahitajika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utaratibu wa kupata fedha kwa ajili ya kukarabati shule hiyo unaendelea ambapo ukarabati mdogo kwenye hosteli na jengo la utawala umefanyika kwa shilingi milioni 17.4. Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kukarabati shule hii kama alivyoelekeza Mheshimiwa Waziri Mkuu.