Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Masache Njelu Kasaka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA K.n.y. MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza:- Je, lini Shule ya Sekondari Kayuki itafanyiwa ukarabati kama alivyoagiza Mheshimiwa Waziri Mkuu?

Supplementary Question 1

MHE. MASACHE N. KASAKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru pamoja na majibu mazuri ya Serikali lakini nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Kwa Mkoa wa Mbeya kuna shule nyingi kongwe ambazo zimechakaa sana zinahitaji ukarabati mkubwa. Je, lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ukarabati wa shule hizi ndani ya Mkoa wa Mbeya lakini na kwa Tanzania kwa ujumla?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili ndani ya Wilaya ya Chunya tuna shule kongwe ambazo zipo toka enzi za mkoloni lakini Serikali ilisema itatoa fedha na mpaka sasa hivi haijatoa fedha kwa ajili ukarabati.

Je, lini Serikali itatoa fedha hizo ili ukarabati uweze kufanyika?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kasaka, kwanza kuhusu shule kongwe lini Serikali itakarabati shule hizi Mkoani Mbeya. Niseme tu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alitafuta fedha kwa ajili ya kuanza ukarabati wa shule kongwe na tayari shule kongwe 84 hapa nchini zimekwisha karabatiwa ikiwemo nyingine zilizo katika Mkoa wa Mbeya. Serikali itaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuendelea na ukarabati wa shule hizi kongwe hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haya maelezo yanaenda pia kwenye swali lake la pili la shule kongwe kule Wilayani Chunya, tutaangalia katika awamu inayofuata ya ukarabati wa shule kongwe tuweze kuweka kipaumbele vilevile katika shule kongwe ambazo zilijengwa na mkoloni kule Wilayani Chunya.

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA K.n.y. MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza:- Je, lini Shule ya Sekondari Kayuki itafanyiwa ukarabati kama alivyoagiza Mheshimiwa Waziri Mkuu?

Supplementary Question 2

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kulitokea changamoto katika shule yetu ya sekondari ya Utemini ambapo ilipelekea sasa kuwahamisha wanafunzi wale wote kuwapeleka kwenye shule zingine Utemini sekondari Mheshimiwa Waziri. Miundombinu haikuwa rafiki katika ufundishaji na Serikali ikawa imeahidi kuleta fedha za kujenga shule ya Utemini sekondari, nataka kujua tu ni lini fedha hiyo itakuja kuhakikisha shule hiyo inajengwa? ahsante sana.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Sima, Serikali kwa sasa imetenga shilingi bilioni 63 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya za sekondari katika kila Halmashauri hapa nchini. Muda si mrefu Waheshimiwa Wabunge wataona katika Halmashauri zao shilingi milioni 570 ndiyo minimum ambayo itapelekwa kwa sababu tumeangalia na uwiano wa maeneo na gharama za ujenzi, lakini minimum inakwenda shilingi milioni 570 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa shule za sekondari mpya ikiwemo hizi za katika Manispaa ya Singida.

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. MASACHE N. KASAKA K.n.y. MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza:- Je, lini Shule ya Sekondari Kayuki itafanyiwa ukarabati kama alivyoagiza Mheshimiwa Waziri Mkuu?

Supplementary Question 3

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona. Tarafa ya Hagati ina shule ya Sekondari ya Hagati ni shule kongwe.

Je ni lini Serikali itatenga fedha na kuikarabati shule hii?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyokuwa nimeshasema kwenye maelezo yangu ya awali. Serikali hii ya Awamu ya Sita ilikuwa imeshatenga fedha ya kukarabati shule kongwe 89 kote nchini na hiyo ilikuwa ni katika awamu ya kwanza na bado Serikali inatafuta fedha kwa ajili ya ukarabati wa shule zingine kongwe ikiwemo hii Shule ya Hagati iliyopo kule Jimboni kwa Mheshimiwa Kapinga.