Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 41 Water and Irrigation Wizara ya Maji 536 2023-06-06

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza:-

Je, lini Serikali itapeleka fedha za utekelezaji wa Miradi ya Maji katika maeneo ya Mkunda Kaengesa, Kaoze Group na Ilemba Kwela?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Jimbo la Kwela, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeanza utekelezaji wa miradi ya maji ya Mkunda Group, Kaoze Group na Ilemba. Miradi hiyo inatarajiwa kukamilika katika mwaka wa fedha 2023/2024 na kunufaisha wananchi wa vijiji vya Mkunda, Kaengesa A, Kaengesa B, Kianda, Ilemba A, Ilemba B, Kaswepa na Kaoze.