Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka fedha za utekelezaji wa Miradi ya Maji katika maeneo ya Mkunda Kaengesa, Kaoze Group na Ilemba Kwela?

Supplementary Question 1

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, Serikali ilifanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina katika Mradi wa Kalole Group utakaohudumia Kijiji cha Skaungu, Kazi, Katonto na Kalole: Je, ni lini Serikali itaanza kujenga mradi huu? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Serikali iliahidi kupitia Mradi wa MAU kuchimba visima kwenye mji mdogo wa Laela na Mpui ambapo kuna changamoto kubwa ya maji. Nataka kujua, hivyo visima vya dharura mtaanza kuchimba lini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Deus Sangu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Mradi wa Kaole sisi kama Wizara tumeshajipanga kwa mwaka ujao wa fedha tutakwenda kuutekeleza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili, maeneo haya mawili ya Laela na Mpui, Mradi wa MAU unaendelea kufanya kazi kwa maana taratibu zinaendelea kukamilishwa na tayari kwa pale Laela utaratibu umekamilika na mwezi huu wa Juni mwishoni tutaanza kuutekeleza kwa kuchimba kile kisima. Pale Mpui mkandarasi ambaye ataenda kufanya usanifu ameshapatikana na mwezi huu Juni anakwenda kufanya kazi. Mara baada ya kumaliza usanifu, tutachimba visima hivi tulivyoahidi kwa wananchi. (Makofi)

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka fedha za utekelezaji wa Miradi ya Maji katika maeneo ya Mkunda Kaengesa, Kaoze Group na Ilemba Kwela?

Supplementary Question 2

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Tunaishukuru sana Serikali kwa kuanza kutekeleza miradi ya Vijiji vya Mkongokieyendo, Minyinga pamoja na Sakaa, lakini kwa masikitiko makubwa, mpaka sasa miradi ile imesimama na inasemekana mkandarasi hajalipwa fedha: Ni lini sasa Serikali italipa fedha ili mkandarasi amalizie miradi ile ambayo ina faida kubwa kwa wananchi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mtaturu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, vijiji hivi vyote alivyovitaja Mheshimiwa ni kweli miradi inaendelea na sisi kama Wizara tumeshaanza kulipa wakandarasi. Hapo katikati kidogo fedha hatukuwanayo, lakini tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais, ametupatia fedha tayari na tunaanza kulipa wakandarasi. (Makofi)

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka fedha za utekelezaji wa Miradi ya Maji katika maeneo ya Mkunda Kaengesa, Kaoze Group na Ilemba Kwela?

Supplementary Question 3

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuniona. Naishukuru sana Serikali ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuahidi kupeleka mradi mkubwa wa Shilingi bilioni 42 kwa ajili ya wananchi wa Kinazi A na B na maeneo ya Msingo ambao hawana kabisa majisafi na salama. Je, ni lini Serikali itaanza kutekeleza mradi huu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Issa Mtemvu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza tumshukuru Mheshimiwa Rais. Shilingi bilioni 42 ni mradi mkubwa. Mheshimiwa Mbunge hongera pia kwa kuendelea kufuatilia miradi hii mikubwa ya kimkakati na mradi huu tunaanza kuutekeleza mwaka ujao wa fedha. (Makofi)

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka fedha za utekelezaji wa Miradi ya Maji katika maeneo ya Mkunda Kaengesa, Kaoze Group na Ilemba Kwela?

Supplementary Question 4

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Wananchi wa Kata za Kimuli, Businde na Bugara hupata changamoto sana ya maji hasa tunapoelekea wakati huu wa kiangazi, lakini ni eneo ambalo lina mvua za kutosha: Je, ni nini mkakati wa Serikali wa kujenga matanki makubwa ili wakati wa mvua tuwe tunavuna maji na wakati wa kiangazi kama hiki tunachokiendea wananchi wanaweza kupata maji ili kuondoa adha wanayopitia kuchota maji ambayo ni tope? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Anatropia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kata hizi alizozitaja zina changamoto ya maji na sisi kama Wizara tunafahamu. Ushauri wa kujenga matanki makubwa tunauchukua, lakini vile vile tumejipanga kuhakikisha maeneo haya yote tunakwenda kuyapatia majisafi na salama. (Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka fedha za utekelezaji wa Miradi ya Maji katika maeneo ya Mkunda Kaengesa, Kaoze Group na Ilemba Kwela?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Je, ni lini wananchi wa Kata ya Ng’ang’ange katika Wilaya ya Kilolo watapatiwa fedha ya mradi wa maji au kuchimibwa visima ili waweze kupata majisafi na salama kwa sababu sasa hivi wanatumia maji ya mito? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nakupongeza Mheshimiwa Dkt. Ritta, hata juzi nimekuona ukiwa na Mheshimiwa Waziri Aweso kuhakikisha changamoto ya maji inakwenda kutatuliwa ukiongozana na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo. Vile vile katika kata hii uliyoitaja ya Ng’ang’ange sisi kama Wizara tunafahamu na tunakwenda kupeleka utatuzi kwa kuchimba visima na unafahamu gari tumeshaifikisha, umeiona wewe mwenyewe. Kwa hiyo, kisima hiki kitachimbwa ndani ya mwaka ujao wa fedha. (Makofi)