Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 41 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 540 2023-06-06

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA K.n.y. MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: -

Je, mpango wa kuufanya Mkoa wa Morogoro kuwa ghala la Taifa la chakula umefikia wapi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Antipas Zeno Mgungusi, Mbunge wa Malinyi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali katika kutekeleza mpango wa kuufanya Mkoa wa Morogoro kuwa Ghala la Taifa imeendelea na jitihada za kuendeleza miundombinu ya umwagiliaji ambapo mkoa una jumla ya skimu 233. Aidha, katika mwaka wa fedha 2022/2023 zaidi ya shilingi bilioni 15 zilitengwa kwa ajili ya kuendeleza skimu za umwagiliaji ili kuongeza tija ya uzalishaji wa mazao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile, mkandarasi mshauri wa kufanya upembuzi yakinifu wa Bonde la Kilombero na Ifakara amekwishapatikana ili kupitia taarifa hiyo ya miradi mipya ya umwagiliaji iweze kuanzishwa na kuongeza uzalishaji. Sambamba na hilo, Serikali inaendelea kuboresha huduma za ugani, upatikanaji wa pembejeo sahihi ikiwemo mbegu bora na mbolea na uimarishaji wa miundombinu ya uhifadhi wa mazao baada ya mavuno.