Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Thea Medard Ntara

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA K.n.y. MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, mpango wa kuufanya Mkoa wa Morogoro kuwa ghala la Taifa la chakula umefikia wapi?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. THEA M. NTARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimshukuru Waziri kwa majibu yake. Sasa swali la kwanza, sehemu kubwa ya bonde la Kilombero imechukuliwa kama hifadhi, maeneo ambayo wakulima walikuwa ndio wanalima kupata chakula.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka miradi ya umwagiliaji ya kutosha ili chakula kisipungue?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Kuwa na ghala moja la chakula naona kama ni risk.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza ghala jingine la chakula hasa kuliweka katika mikoa ile inayozalisha sana ikiwemo Mkoa wa Ruvuma?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Katika swali lake la kwanza, katika kuendeleza kilimo cha umwagiliaji katika Mkoa wa Morogoro kupitia bajeti yetu tulitangaza hapa ndani Bungeni kwenye kiambatisho namba tano cha bajeti yetu. Tumelezea vizuri kabisa kwamba Serikali inakwenda kufanya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina wa mabonde ya kimkakati 22, na mabonde matatu yatatoka ndani ya Mkoa wa Morogoro, yaani kwa maana ya bonde la Kilombero ambalo lina hekta 53,340. Tuna bonde la Usangule ambalo linakwenda kuhudumia mpaka Malinyi ambalo lina hekta 2,500 na tuna bonde la Ifakara - Idete ambalo linagusa Wilaya yote ya Kilombero.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo katika eneo lake la Malinyi tunao mradi ambao unaendelea mradi wa Itete wa scheme ya umwagiliaji ambao pia utasaidia kutatua changamoto hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili, Serikali inayo dhamira ya dhati kabisa kuhakikisha ile mikoa mitano ambayo ndio Ghala la Taifa la Chakula kuendelea kuimarisha huduma mbalimbali, hasa katika upatikanaji wa huduma za ugani lakini vile vile na upataikanaji wa pembejeo za mbolea ili wakulima wetu waweze kulima na kuongeza tija, ikiwemo Mkoa wa Ruvuma ambao ni kati ya Mkoa unaofanya vizuri sana kwenye kilimo cha mazao ya chakula.

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA K.n.y. MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, mpango wa kuufanya Mkoa wa Morogoro kuwa ghala la Taifa la chakula umefikia wapi?

Supplementary Question 2

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kunipa fursa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iliongeza zao la parachichi kama zao la kimkakati na katika kutimiza ajenda hiyo, iliamua kuanza ujenzi wa kiwanda kikubwa cha kuchakata parachichi kilichopo Nyololo Mufindi ili isaidie mikoa yote ya Nyanda za juu Kusini. Hata hivyo mpaka sasa hivi ujenzi haujaanza.

Je, ni ipi kauli ya Serikali juu ya mradi huu muhimu sana kwa wananchi wa Mufindi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli katika bajeti yetu ya mwaka 2022, 2023 tuliweka mpango wa kujenga common use facilities mbili. Moja itajenga Wilaya ya Hai Mkoa wa Kilimanjaro na moja inajengwa nyololo Jimboni kwa Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka nimpe taarifa njema Mheshimiwa Mbunge kwamba tumekamilisha taratibu zote za awali na muda si mrefu mkandarasi atapatikana na kazi ya ujenzi wa common use facilities itaanza. Kazi hii ikianza itawapa nafasi wakulima wote wa parachichi kukusanya maparachichi yao sehemu moja, tukafanya collection, tukafanya grading na sorting na baadaye packaging ili maparachichi yetu ya Tanzania ionekane duniani kwamba ni produce of Tanzania kuliko hivi sasa ambapo maparachichi mengi yanakwenda katika nchi za jirani. (Makofi)

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. THEA M. NTARA K.n.y. MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza: - Je, mpango wa kuufanya Mkoa wa Morogoro kuwa ghala la Taifa la chakula umefikia wapi?

Supplementary Question 3

MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Ni kwamba maghala mengi yamejengwa maeneo ambayo mikoa inazalisha chakula, tunakubaliana nayo. Lakini pale kuna mikoa mingine uzalishaji wa chakjula ni kidogo sana na mvua ni za shida. Inapotokea shida ya chakula kunakuwa tena kuna gharama ya kusafirisha; gharama ya fedha na gharama ya muda kutoka maeneo yanayozalisha chakula kwenda kwenye maeneo yasiyozalisha chakula.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuweka maghala vile vile katika maeneo ambayo mikoa inazalisha kidogo chakula kama Mkoa wa Simiyu na hasa maeneo amabayo yana shida ya chakula? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti yetu ambayo inamalizikia tumetenga shilingi 25 kwa ajili ya ujenzi wa maghala na tumeangalia maeneo yote. Kwa mfano katika Mkoa wa Simiyu hivi sasa kupitia mradi wa TANIPAC wa sumu kuvu tumebadilisha matumizi ya ghala lile ili ibaki kuwa sehemu ya ghala kuhudumia Mkoa wa Simiyu na mikoa Jirani ambao uzalishaji wake si mkubwa sawa na mazao ya chaklula ili inapotokea changamoto ya chakula cha msaada basi tuweze kukipeleka kwa uharaka zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tumezingatia pia jiografia hiyo na uzalishaji katika maeneo husika.