Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 41 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 542 2023-06-06

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: -

Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Barabara za Itoni – Ludewa – Manda na Mkiu – Liganga – Madaba kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Zacharius Kamonga, Mbunge wa Ludewa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Itoni – Ludewa – Manda yenye urefu wa kilometa 211.42 inajengwa kwa kiwango cha zege kwa awamu. Hadi sasa, Serikali imekamilisha Sehemu ya Lusitu – Mawengi kilomita 50. Kwa sehemu ya Itoni – Lusitu kilomita 50 kazi za ujenzi kwa kiwango cha zege zinaendelea. Kwa sehemu iliyobaki ya kutoka Mawengi – Manda kilomita 98.1, Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Barabara ya Mkiu – Liganga – Madaba yenye urefu wa kilomita 112 inayounganisha barabara ya Itoni – Ludewa hadi Manda na barabara kuu ya Makambako – Songea katika maeneo ya Mkiu na Madaba Mtawalia, tayari imefanyiwa upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ikihusisha sehemu ya Liganga Nkomangómbe kilomita 70 na Nkomangómbe – Coal Power kilomita 4.14. Kwa sasa Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi, ahsante.