Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Zacharius Kamonga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Barabara za Itoni – Ludewa – Manda na Mkiu – Liganga – Madaba kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na shukrani nyingi kwa Serikali kwa kukamilisha kipande cha Lusitu - Mawengi na kuanza kipande cha Itoni – Lusitu ambapo kipande kile cha mwanzo kilitumia bilioni 179 cha pili bilioni 90 bado ninaomba kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza, pale Mawengi wakati wanajenga ile barabara kuna wananchi wachache ambao hawakulipwa fidia wamekuwa wakihangaika sana;

Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi wale ili waache kuhangaika?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ningepena kufahamu Serikali imejenga barabara nyingi Ludewa lakini haijaweka taa za barabarani;

Je, ni lini Serikali itakwenda kuweka taa za barabarani hasa maeneo yenye miji ambayo yana wananchi, ili mji wetu uweze kuonekana wa kisasa zaidi? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Kamonga Mbunge wa Ludewa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu fidia; wananchi hawa ni kweli walikuwa hawajalipwa na ni kwa sababu zoezi wakati la ulipaji linaendelea hawa wananchi hawakuwepo. Nimuombe Mheshimiwa Mbunge na wananchi hao waweze kumuona Meneja wa Mkoa wa Njombe ili aweze kuwapa taratibu zitakazofanyika namna ya kuwalipa wananchi hawa ambao walipisha ujenzi wakati wa mradi huu, hawa wananchi wa Mawengi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kuhusu taa za barabarani. Kama tulivyosema sehemu zote za wilayani na kwenye miji ama center kubwa ni mpango sasa wa Serikali kuhakikisha kwamba tunaweka taa za barabarani. Na katika mwaka wa fedha ujao nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge moja ya eneo ambalo litafaidika kuwekewa taa ni pamoja na mji wa Ludewa, ahsante.

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Barabara za Itoni – Ludewa – Manda na Mkiu – Liganga – Madaba kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa fursa. Je, Serikali ina mkakati gani wa kukamilisha barabara ya Kibosho Shine hadi kwa Rafael kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Prof. Ndakidemi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara aliyoitaja ya Kibosho Shine kwenda kwa Rafael ina hudumiwa na Wakala wa Barabara Tanzania lakini kuna kipande ambacho pia kinahudumiwa na wenzetu wa TARURA. Kwa upande wa barabara ambayo kwa sasa inahudumiwa na TANROADS ni mpango wetu kuhakikisha kwamba tunaijenga yote kwa kiwangio cha lami, na hadi sasa mkandarasi yuko site. Na katika mwaka unaokuja pia tumetenga fedha kuendelea na ujenzi kwa awamu kwa kiwango cha lami ili kuikamilisha barabara yote hiyo kuijenga kwa kiwango cha lami.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH Z. KAMONGA aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Barabara za Itoni – Ludewa – Manda na Mkiu – Liganga – Madaba kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza;

Je, lini Serikali itakamilisha barabara ya kutoka Mji Mwema mpaka Pemba Mnazi ni ya muda mrefu sana?

Je, lini sasa itakamilisha kipande cha kutoka Gomvu mpaka Pemba Mnazi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nataka kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilishafanya taratibu na tuko kwenye hatua za manunuzi kwa maana ya kujenga barabara ya kilometa 41 kwa kiwango cha lami. Barabara ambayo ametaja kilometa 41.