Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 41 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 543 2023-06-06

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MWITA W. WAITARA aliuliza: -

Je, lini ujenzi wa barabara ya Tarime – Mugumu utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mwita Mwikwabe Waitara, Mbunge wa Tarime Vijijini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeanza ujenzi wa Barabara ya Tarime – Mugumu kilomita 87.14 kwa kiwango cha lami kwa awamu. Ujenzi kwa kiwango cha lami awamu ya kwanza sehemu ya Mogabiri – Nyamongo kilomita 25 unaendelea na utekelezaji wake umefikia asilimia 15. Aidha, Serikali ipo katika hatua za mwisho za manunuzi za kumpata Mkandaraasi atakayetekeleza ujenzi wa sehemu ya pili ya kutoka Tarime Mjini – Mogabiri na Nyamongo hadi Mugumu zenye jumla ya kilometa 62.14.