Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. MWITA W. WAITARA aliuliza: - Je, lini ujenzi wa barabara ya Tarime – Mugumu utaanza?

Supplementary Question 1

MHE. MWITA W. WAITARA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii barabara inaunganisha Wilaya ya Tarime na Wilaya ya Serengeti na ndiyo barabara ya kwanza ya lami katika Jimbo la Tarime Vijijini. Tunampongeza Mheshimiwa Rais kupeleka fedha hapa kujenga barabara hii. Lakini kwa majibu ya Serikali barabara hii imefika asilimia 15, na tumeambiwa Tarehe 24 Mwezi wa Januari Mwaka kesho tunakabidhiwa barabara ya lami. Lakini mkandarasi alipeleka certificate Serikalini Oktoba 2022 akidai milioni 874, hajalipwa. Akapeleka certificate ya pili Machi 2023 akidai milioni 841, hajalipwa. Certificate ya tatu ni Mwezi wa tatu mwaka huu ambayo ni bilioni 1.6.

Je, ni lini, Serikali italipa fedha hizi ili tupate barabara ile Januari mwakani kutengeneza kura za Chama Cha Mapinduzi katika jimbo langu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Barabara hii ina center ya Mogabiri, center ya Nyamwigora, center ya Kimakolele, center ya Nyarero, center ya Kiwanja, center ya Gena na kule Nyamongo;

Je, maeneo haya tutawekewa taa za barabarani? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na swali la pili la Mheshimiwa Mbunge swali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tulivyosema katika barabara hii ya Tarime – Nyamwaga – Nyamongo hadi Mugumu, tumeainisha maeneo sita ambayo yatawekwa taa. Yale maeneo yote, vijiji vyote vile vikubwa, maeneo sita yatawekewa taa na Mheshimiwa Mbunge pengine baada ya hapa anaweza kuja nimwoneshe vijiji ambavyo vitawekewa taa katika hiyo barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ujenzi unaoendelea, mkandarasi bado yupo site anaendelea kujenga na tuna hakika changamoto iliyokuwepo kubwa ya barabara hii ni mvua kubwa inayoendelea kunyesha. Sasa Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba, kasi ya ujenzi itaendelea na hasa kwa kuwa Serikali sasa tumeshajipanga kuhakikisha kwamba, changamoto zilizokuwepo za malipo yote tunakamilisha na mkandarasi ataendelea na ujenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, kipande kilichobaki tunategemea ikiwezekana kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha tutakuwa tumesaini mkataba kwa ajili ya barabara nzima hiyo ya Tarime – Nyamwaga hadi Mugumu. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. MWITA W. WAITARA aliuliza: - Je, lini ujenzi wa barabara ya Tarime – Mugumu utaanza?

Supplementary Question 2

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniruhusu niulize swali la nyongeza. Barabara ya Tegeta – Basihaya – Bunju mpaka Bagamoyo katika Jimbo la Kawe imejengwa bila mitaro ya maji. Kwa sababu hiyo, husababisha mafuriko makubwa sana kwenye maeneo ya Nyaishozi, Tegeta, Nyamachabes. Sasa, ni lini Serikali itajenga mitaro ya maji kuepusha hatari kwa wananci kwa sababu ya mvua zinazoendelea?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, Askofu Gwajima, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli tunatambua katika kipindi hiki mvua imeendelea kubwa sana kwa Jiji la Dar-es-Salaam na eneo alilolitaja kwa kweli limeathirika kwa kiasi kikubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo aliyoyataja yote ya Basihaya, Msikitini, DAWASA na Nyaishozi yalikuwa yamefanyiwa design yaanze kujengwa kabla, lakini kwa kuwa tuna Mradi mkubwa wa BRT IV maeneo haya yatakuwa ni sehemu ya ujenzi wa Mradi huo wa BRT IV.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge pamoja na wananchi wa Jimbo la Kawe, tulichokifanya, tutawahusisha na tumehusisha pia TARURA ili wakati wa kujenga pia hiyo mitaro na wenzetu wa TARURA tusije tukajenga halafu kuwe na changamoto kwenye barabara zetu, kwa hiyo nao watahusika. Mkataba uko tayari kusainiwa. Kwa hiyo, muda wowote kazi ya ujenzi kwa BRT IV itaanza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini? Inawezekana hata ikawa Juni tukasaini huo mkataba. Ahsante. (Makofi)