Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 44 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 568 2023-06-09

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: -

Je, kuna mkakati gani wa kufanya mageuzi ya kilimo nchini?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo napenda kujibu swali la Mheshimiwa Abeid Ramadhani Ighondo, Mbunge wa Singida Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza mikakati mbalimbali wa kuleta mageuzi ya kilimo. Mikakati hiyo inatekelezwa kwa lengo la kubadili kilimo kutoka kilimo cha kujikimu kuwa kilimo biashara, chenye tija, himilivu kinachoratibiwa na kusimamiwa na Serikali na kushirikisha sekta binafsi ili kuwa na mifumo endelevu ya chakula na kilimo.

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia misingi hiyo ya kuleta mageuzi katika sekta ya kilimo, Serikali kupitia bajeti ya mwaka 2023/2024 inatekeleza vipaumbele mikakati yenye lengo la kuongeza tija na uzalishaji; kuongeza ajira zenye staha na ushiriki wa vijana na wanawake kwenye kilimo; kuimarisha usalama wa chakula na lishe; kuimarisha upatikanaji wa masoko, mitaji na mauzo ya nje ya nchi na kuimarisha maendeleo ya ushirika.