Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kufanya mageuzi ya kilimo nchini?

Supplementary Question 1

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, pamoja na majibu haya mazuri ya Serikali ninayo maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwanza je, Serikali sasa ina mpango gani mahususi wa kuwapatia wakulima nchini zana za kisasa za kilimo hususani matrekta ambapo sasa hivi tunaona wananchi wetu wanatumia jembe la mkono katika maeneo mbalimbali?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Serikali ina mpango gani mahususi wa kufanya kilimo cha umwagiliaji kuwa ni ajenda ya kitaifa ambapo wananchi wetu sasa waweze kulima mara mbili kwa mwaka kuondokana na kilimo cha kutegemea mvua. Tuna maeneo mengi yenye maji kama Singida Kaskazini, lakini bado hayajatumiaka ipasavyo. Tunaomba mkakati mahsusi wa Serikali kuhusu ku–mechanize kilimo chetu.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, nikianza na swali la kwanza la Mheshimiwa Mbunge kuhusu zana za kilimo kama alivyosema tunaendela kufanya mageuzi katika matumizi ya zana za kilimo za kisasa ili wakulima wetu waweze kuzalisha kwa tija na hivi sasa tunashirikiana na CARMTEC na Shirika la TEMDO katika kuja na teknolojia mbalimbali na zana mbalimbli za kusaidia katika uzalishaji katika sekta hii ya kilimo. Lakini kubwa kuliko yote ni kwamba tunakwenda kuanzisha mechanization hub katika ikolojia mbalimbali za nchi yetu ya Tanzania kikanda ili wakulima wetu pia waweze kutumia fursa hiyo ya kuweza kutumia mitambo hiyo ya kukodisha badala ya mkulima kwenda kukopa trekta huko ana ekari mbili na kuingia gharama kubwa, tunaweka vituo hivi kwa ajili ya ukodishaji wa zana za kilimo za kisasa.

Mheshimiwa Spika, la pili kuhusu mipango mahususi katika eneo la umwagiliaji, kama nilivyokuwa nikisema hapa ndani ni dhamira ya Serikali kuhakikisha ya kwamba tunatekeleza kwa dhati kabisa eneo hili la umwagiliaji kwa kuweka mipango madhubuti na mkakati mkubwa hivi sasa ni kuhakikisha scheme zetu zote za umwagiliaji nchini zinafanya kazi, lakini hatua kubwa na ya kwanza ni kuhakikisha kwanza tunaweka vyanzo vya uhakika vya maji ili scheme hizo ziweze kufanya kazi na wananchi waweze kuhudumia mashamba yao zaidi ya mara moja ndani ya mwaka mmoja.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kufanya mageuzi ya kilimo nchini?

Supplementary Question 2

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi, pamoja na mkakati uliosema wa kugeuza kilimo kama cha biashara.

Je, kuna mkakati gani kwenye eneo la Yaeda Chini na Eshkesh ambayo ni kame unavyojua kuyageuza maeneo hayo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, tunakwenda kuanzisha ukanda wa kilimo wa kikanda nchi nzima ili kuweza kuyafikia maeneo yote kutokana na ikolojia, kwa hiyo, na maeneo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyataja kupitia utaratibu huu tutaweza kuyafikia na kuwasaidia wakulima wetu kulima kwa tija.

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO aliuliza: - Je, kuna mkakati gani wa kufanya mageuzi ya kilimo nchini?

Supplementary Question 3

MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Spika, Serikali ina mikakati gani ya kuhakikisha kuwa mbolea na pembejeo za kilimo zitafika mapema kabla ya mvua za mwanzo hazijanyesha? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, Serikali imekwisha kutamka narudia tena huku kwamba tutahakikisha wakulima wetu hawapati changamoto zilizojitokeza katika msimu uliopita, mbolea ya kupandia na kukuzia itaanza kuingia mwezi wa saba mapema kabisa ili wakulima waweze kununua na uhifadhi kwa ajili ya msimu unaokuja. (Makofi)