Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 44 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 569 2023-06-09

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha umeme unafika kwenye vitongoji vyote nchini?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati napenda kujibu swali la Mheshimiwa Jafari Wambura Chege, Mbunge wa Rorya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imekamilisha uhakiki wa vitongoji 36,101 visivyokuwa na huduma ya umeme na kuandaa mradi kabambe wa kusambaza umeme katika vitongoji vyote uliopewa jina Hamlet Electrification Project (HEP) vikiwemo vijiji 262 vya Wilaya ya Rorya. Mradi huu utagharimu takribani shilingi 6,700,000,000,000.

Mheshimiwa Spika, Serikali inakamilisha mipango ya upatikanaji wa fedha hiyo na mradi huu unatarajiwa kutekelezwa ndani ya miaka mitano kuanzia mwaka wa fedha 2024. Aidha, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Jimbo la Rorya litapatiwa fedha kutoka REA ya kufikisha umeme katika vitongoji 15 vya kuanzia, nashukuru.