Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha umeme unafika kwenye vitongoji vyote nchini?

Supplementary Question 1

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi, nataka nijue ni lini sasa REA Phase Three Round Two ya kusambaza kilometa mbili za ziada kwenye Wilaya ya Rorya utaanza kufanya kazi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini swali langu la pili. Kampuni tanzu ya ETDCo imepewa kazi zaidi ya miaka mitatu sasa kusambaza umeme wilaya ya Rorya, lakini mpaka sasa hawajaanza kufanya kazi.

Je, Serikali haioni sasa kuna umuhimu wa kumfuta mkandarasi huyu ili itangaze upya waombe wakandarasi wengine kwa ajili ya kusambaza umeme Wilaya ya Rorya?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, leo tunatarajia wenzetu wa REA watasaini baadhi ya mikataba ya extension ya kilomita mbili kwa kila kitongoji na tunaamini kufikia mwishoni mwa mwezi huu wakandarasi hao watafika site ili kuanza kufanya kazi hizo za kuongeza hizo kilometa mbili kwenye maeneo ambayo mikataba ya vijiji imekamilika na pengine inaendelea.

Mheshimiwa Spika, kwenye eneo la pili, naomba baada ya hapa nikae na Mheshimiwa Chege ili tuone tatizo liko wapi kwa sababu tunafahamu miradi mingi inaendelea kwa hatua mbalimbali katika maeneo yetu, specifically nitakaa ili tubaini changamoto aliyoiona iko wapi na tuweze kueleweshana na kuchukua hatua stahiki.

Name

Margaret Simwanza Sitta

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Urambo

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha umeme unafika kwenye vitongoji vyote nchini?

Supplementary Question 2

MHE. MARGARET S. SITTA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kunipa nafai hii.

Je, Serikali itamaliza lini ujenzi wa kituo cha kupozea umeme kinachojengwa katika Kijiji cha Uhuru, wilayani Urambo ili kumaliza tatizo la umeme tulilonalo? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, mradi wa kujenga kituo cha kupoza umeme cha Uhuru kilichoko Urambo ni mojawapo ya miradi yetu 14 ya kujenga vituo vya kupoza umeme kwenye Wilaya inayotekelezwa chini ya mradi wetu wa Gridi Imara. Mradi huo tayari umeshaanza na tunatarajia ndani ya miezi kama 12 kuanzia sasa mradi huo pia utakuwa umekamilika katika eneo la Uhuru ili kuhakikisha kwamba umeme unaotoka Tabora kwenda Uhuru kwenda Nguruka basi unawafikia wahitaji kwa wakati.