Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 44 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 572 2023-06-09

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaunga mkono juhudi za ujenzi wa Kituo cha Polisi Wilaya ya Liwale?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zuberi Mohamed Kuchauka, Mbunge wa Liwale kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Liwale imetoa eneo lenye ukubwa wa mita za mraba 10,000 kwa ajili ya kujenga Kituo cha Polisi pamoja na nyumba za makazi ya askari. Tathmini ya makadirio na michoro kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Polisi, daraja B umeshafanyika na kiasi cha Sh.768,024,734/= kinahitajika. Fedha hizo zitatolewa kwenye Mfuko wa Tuzo na Tozo katika mwaka wa fedha 2023/2024, nakushukuru.