Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaunga mkono juhudi za ujenzi wa Kituo cha Polisi Wilaya ya Liwale?

Supplementary Question 1

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, kwanza nishukuru kwa mara ya kwanza swali langu hili limepata majibu mazuri ya Serikali, imenitia tumaini, lakini bado ina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa sababu ya kituo hiki kuitwa kituo cha karibu cha usaidizi Mheshimiwa Waziri Mkuu alipokuja Liwale alituahidi kutujengea kituo kwenye Tarafa ya Kibutuka na Kata ya Lilombe. Je, ahadi hiyo itatekelezwa lini?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa sababu jiografia ya Liwale kuwa ngumu hali ya usafiri ni mbaya sana, sasa je, Serikali iko tayari kutupatia gari kwa ajili ya maaskari wa kituo hiki?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, najibu maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nataka nimwambie Mheshimiwa Mbunge kuchauka kwamba ahadi zote zilizoahidiwa na viongozi wa Serikali zitatekelezwa. Sasa hivi tupo kwenye kufanya tathmini kuona wapi paliahidiwa ili tuanze sasa utekelezaji wa ahadi hizo. Kwa hiyo hicho ambacho kimeahidiwa Mheshimiwa awe na amani kitatekelezwa.

Mheshimiwa Spika, kingine nimwambie ni kweli Serikali inafahamu umuhimu wa uwepo wa magari katika meneo mengi ambayo watu wanaishi kwa ajili ya kuhakikisha kwamba, kwanza tunafanya operation za mara kwa mara, lakini kufanya doria za mara kwa mara na kuhakikisha kwamba tunapambana na matukio ya kihalifu. Nimwambie tu Mheshimiwa kwamba katika gari ambazo zitafika tutahakikisha kwamba katika Jimbo la Liwale gari itakwenda ili iweze kusaidia wananchi kwa ajili ya kuweka hali ya amani na utulivu katika eneo hilo, nakushukuru.

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaunga mkono juhudi za ujenzi wa Kituo cha Polisi Wilaya ya Liwale?

Supplementary Question 2

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa fursa. Serikali imepeleka Polisi Kata kwenye kila Kata katika nchi hii kwenye rank ya inspector, lakini mapolisi hawa hawana ofisi wala makazi kwenye haya maeneo. Je, Serikali ina mpango gani kuwapelekea vijana wetu hawa kuwajengea Ofisi na nyumba za kuishi?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, ni kweli tunatambua kwamba kuna baadhi ya Ofisi zimekuwa zimechakaa kwa sababu ni za muda mrefu, lakini vilevile tunatambua kwamba kuna maeneo mengine hata hizo Ofisi zinakuwa changamoto, lakini nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tutajitahidi, kama ambavyo tumejibu katika majibu yetu ya msingi, tutajitahidi kuhakikisha kwamba kila mahali wanapata Vituo vya Polisi, lakini kila mahali wanapata nyumba za makazi kwa ajili ya Askari Polisi, nakushukuru.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaunga mkono juhudi za ujenzi wa Kituo cha Polisi Wilaya ya Liwale?

Supplementary Question 3

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Je, ni lini Serikali itawajengea askari polisi wa Wilaya ya Kilolo kwa sababu hawajawahi kujengewa nyumba, wanaishi kwenye nyumba za kupanga? (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimeanza kutoa maibu yangu kwamba, tutahakikisha katika bajeti ambayo tumeeleza hapa katika jibu letu la msingi, tutahakikisha kwamba tunaanza ama tunaendeleza kujenga nyumba za makazi, kwa sababu kama tulivyosema mwanzo hiyo changamoto tunaifahamu na tunajua kwamba askari wetu wengi wanaishi kwenye nyumba nyingi zimechakaa, lakini tutahakikisha kwamba tunawajengea nyumba na makazi ya kisasa ili waweze kukaa kwenye makazi mazuri na kuweza kutoa huduma vizuri kwa wananchi.