Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 44 Water and Irrigation Wizara ya Maji 573 2023-06-09

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza:-

Je, ni lini Wananchi wa Mpiji – Magohe, Kibesa, Msumi, Makabe, Msingwa, Ukombozi na Goba watapata majisafi na salama?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Issa Jumanne Mtemvu, Mbunge wa Kibamba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inaendelea na ukamilishaji wa Miradi ya Maji ya Changanyikeni - Bagamoyo, ujenzi wa matenki ya maji katika maeneo ya Mshikamano, Tegeta A, Malolo na mradi wa usambazaji maji kusini mwa Dar es Salaam ambapo kukamilika kwa miradi hii kutawezesha wakazi wa maeneo ya Mpiji-Magohe, Kibesa, Msumi, Mbezi, Makabe, Msakuzi, Msingwa, Ukombozi, King'azi, Malamba Mawili, Msingwa, Kipesa Mapwepande, Mpakani na Goba kupata huduma ya majisafi, salama na ya kutosheleza.