Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza:- Je, ni lini Wananchi wa Mpiji – Magohe, Kibesa, Msumi, Makabe, Msingwa, Ukombozi na Goba watapata majisafi na salama?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, ni dhahiri nimshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa utekelezaji wa miradi hii iliyotajwa na Serikali, tunawashukuru sana Serikali. Pamoja na changamoto sasa iliyopo tayari miradi ya Tegeta A na Mshikamano tunayo mizuri usambazaji wa mabomba umekuwa ni changamoto sana kwa sababu ya yale maboza, magari yanayouza maji kwa wananchi…

SPIKA: Swali lako Mheshimiwa.

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali kwa sababu tayari wanatakiwa wasambaze watoe kauli hapa ya kusitisha uuzaji wa maji kwa magari. Hilo ni swali la kwanza.

Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa kuna mradi huo wa usambazaji maji…

SPIKA: Mheshimiwa Issa Mtemvu, hebu ngoja kwanza, Naibu Waziri kwa sasa hivi hasikilizi mchango, anataka swali ili akujibu kwa sababu hiki ni kipindi cha maswali na majibu. Muulize swali Naibu Waziri akujibu.

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, swali la kwanza Serikali mpo tayari kutoa kauli ya usitishaji wa uuzaji wa maji kwa magari Jimbo la Kibamba kwa sababu mlishatekekeleza miradi miwili kule?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa sababu King’azi hakuna maji kabisa wanatumia maji ya chumvi, ni lini mradi wa usambazaji Dar es Salaam Kusini utaanza?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mtemvu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na uuzaji wa maji kwenye magari hili suala tulishalipigia marufuku kwa maeneo mengi na hususani eneo la Kibamba, lakini tutaendelea kuhakikisha kwanza tunahakikisha miradi ile imekamilika na uhakika wa maji ya uhakika wa kila siku kwa wananchi, suala hili naamini litatekelezeka.

Mheshimiwa Spika, suala la Dar es Salaam kusini maeneo ya King’azi usambazaji wa mabomba, tunatarajia mapema mwaka wa fedha ujao kuanzia mwezi Julai au Agosti, suala la usambazaji wa mabomba katika maeneo haya yote aliyoyataja Mheshimiwa Mbunge tunakuja kuyafanyia kazi.

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza:- Je, ni lini Wananchi wa Mpiji – Magohe, Kibesa, Msumi, Makabe, Msingwa, Ukombozi na Goba watapata majisafi na salama?

Supplementary Question 2

MHE FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa ya kuuliza swali la nyongeza. Jiji la Dodoma limekuwa lina matatizo sana ya upatikanaji wa maji na hivyo kuwa kero kubwa sana kwa wananchi. Je, ni nini mkakati wa Serikali wa kupunguza tatizo hili ili kusudi wananchi waweze kufaidika na maji safi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Fatma Toufiq, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Dodoma, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali kwa Jiji la Dodoma Waheshimiwa Wabunge naamini ni mashahidi tunaendelea kufanya kazi nyingi sana kuona tunakwenda kukomesha tatizo la maji katika Jiji la Dodoma kwa umuhimu wake kama Makao Makuu ya Nchi tuna miradi mingi mikubwa, ya kati na midogo, tunatarajia mwaka ujao wa fedha miradi mingi itaanza kupeleka huduma ya maji maeneo yote ambayo yanapata changamoto.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza:- Je, ni lini Wananchi wa Mpiji – Magohe, Kibesa, Msumi, Makabe, Msingwa, Ukombozi na Goba watapata majisafi na salama?

Supplementary Question 3

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itakamilisha miradi ya maji katika Kata ya Duru na Yasanda, Jimbo la Babati Vijijini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asia, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, maeneo ya Babati Vijijini, Miradi ambayo ipo kwenye utekelezaji tunaendelea kupambana kuona inakamilika ndani ya wakati na maeneo ambayo usanifu umekamilika pia mwaka ujao wa fedha tutaendelea kuongeza nguvu katika maeneo yote ya Babati Vijijini ili kupata maji safi na salama.

Name

Shabani Hamisi Taletale

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza:- Je, ni lini Wananchi wa Mpiji – Magohe, Kibesa, Msumi, Makabe, Msingwa, Ukombozi na Goba watapata majisafi na salama?

Supplementary Question 4

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kuuliza, je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya maji katika Tarafa ya Ngerengere?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hamisi Taletale, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Tarafa ya Ngerengere tayari tuna miradi ambayo ipo kwenye utekelezaji, lakini tuna mipango thabiti ya kuona kwamba eneo hili nalo linaenda kupata huduma ya maji safi na salama mwaka ujao wa fedha Mheshimiwa Mbunge atashuhudia shughuli nyingi sana zikifanyika katika Tarafa hii.

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza:- Je, ni lini Wananchi wa Mpiji – Magohe, Kibesa, Msumi, Makabe, Msingwa, Ukombozi na Goba watapata majisafi na salama?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Je, ni lini Wizara ya Maji itaanza kujenga au kutekeleza Mradi wa Maji kutoka Ziwa Victoria kwa ajili ya Wilaya ya Muleba?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Kikoyo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mradi wa Ziwa Victoria kwa Muleba Mheshimiwa Mbunge alikuja tukaongea na menejimenti, tulishakubaliana mwaka ujao wa fedha tunakwenda kukamilisha usanifu na kuanza kuona uwezekano wa kufanya mradi huu.

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza:- Je, ni lini Wananchi wa Mpiji – Magohe, Kibesa, Msumi, Makabe, Msingwa, Ukombozi na Goba watapata majisafi na salama?

Supplementary Question 6

MHE. HASSAN Z. KUNGU: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, ni lini Serikali itapeleka Mradi wa Maji katika Kata ya Kalulu na Kata ya Jakika? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Kata hizi alizozitaja mwaka ujao wa fedha tunatarajia kupeleka maji safi na salama kwa kupitia visima vilevile maeneo mengine tutatumia vyanzo vile vilivyo vya uhakika.