Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 44 Water and Irrigation Wizara ya Maji 574 2023-06-09

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:-

Je, upi mpango wa Serikali kumaliza kero ya upatikanaji wa maji safi na salama Wilayani Ukerewe?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Michael Mkundi, Mbunge wa Jimbo la Ukerewe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Ukerewe ina jumla ya vijiji 76, kati ya vijiji hivyo 37 vinapata huduma ya maji safi na salama. Aidha, katika mwaka 2022/2023, Serikali inatekeleza miradi katika vijiji vingine 26 na inatarajia kukamilisha miradi hii mwezi Julai, 2023.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024 Serikali itajenga miradi ya maji kwenye vijiji 13 vilivyobaki ambapo ni Bugula, Kameya, Halwego, Chamuhunda, Mukunu, Bugorola, Kamasi, Busumba, Kaseni, Bukonyo, Busagami, Msozi na Kweru. Kukamilika kwa miradi hiyo kutaondoa kero ya maji Wilaya ya Ukerewe na wananchi wote watapata huduma ya maji safi, salama na yenye kutosheleza. (Makofi)