Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:- Je, upi mpango wa Serikali kumaliza kero ya upatikanaji wa maji safi na salama Wilayani Ukerewe?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Nitumie nafasi hii kwanza kutoa pongezi na shukurani kwa Wizara pamoja na Serikali kwa ujumla kwa hatua mbalimbali zinazofanyika kuhakikisha Visiwa vya Ukerewe vinapata maji safi na salama. Swali langu, Serikali sasa iko tayari kutoa maelekezo ili wakati wa usambazaji wa maji wataalam wazingatie mtawanyo kuhakikisha kwamba kila kitongoji kinafikishiwa mtandao huu wa maji? Nashukuru sana.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Joseph Mkundi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwanza napokea shukrani zako na wewe nakupongeza kwa sababu umekuwa mfuatiliaji na tumekwenda Ukerewe zaidi ya mara mbili mimi na wewe na kazi nzuri unaifanya.

Mheshimiwa Spika, suala la usambazaji maji kwa kila kitongoji, hiyo ni moja ya mipango ya Wizara. Nikutoe hofu Mheshimiwa Mbunge kama ambavyo tumeweza kutatua changamoto ambayo ilikutesa kwa muda mrefu, suala la usambazaji maji pia tunakuja kulifanyia kazi na nitoe wito kwa Mameneja wote wa Wilaya ambao wananisikiliza waweze kuhakikisha wanafika katika vitongoji vyote na maji yanasambazwa kadri ya miradi ilivyosanifiwa. (Makofi)

Name

Salome Wycliffe Makamba

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:- Je, upi mpango wa Serikali kumaliza kero ya upatikanaji wa maji safi na salama Wilayani Ukerewe?

Supplementary Question 2

SALOME W. MAKAMBA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Mheshimiwa Spika, Serikali ilipanga kupeleka shilingi bilioni 195 ili kumaliza changamoto ya maji katika Mkoa wa Shinyanga. Nataka kujua Serikali imefikia wapi kutekeleza mpango huu? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Salome Makamba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuleta shilingi bilioni 195 katika eneo la Shinyanga ni miradi ya kimkakati ambayo Wizara tunaendelea kutafuta fedha. Mara tutakapopata fedha tutaendelea kuzileta kwa awamu ili kuhakikisha mradi huu unatekelezeka. (Makofi)

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:- Je, upi mpango wa Serikali kumaliza kero ya upatikanaji wa maji safi na salama Wilayani Ukerewe?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kuna changamoto kubwa sana ya upatikanaji wa maji katika Kata ya Bonyokwa Jimbo la Segerea. Je, ni lini changamoto hii itakwisha? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecilia Paresso, Mbunge Viti Maalum kuwa maeneo ya Segerea, Bonyokwa tuna miradi ambayo iko mwishoni kabisa kukamilika, tunatarajia mapema mwaka wa fedha ujao maeneo haya yote yanakwenda kupata huduma ya maji safi na salama.

Name

Dr. Tulia Ackson

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:- Je, upi mpango wa Serikali kumaliza kero ya upatikanaji wa maji safi na salama Wilayani Ukerewe?

Supplementary Question 4

SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, mradi wa maji Kiwira unaanza lini? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwa umuhimu kabisa naomba kujibu swali hili kwa heshima kubwa.

Mheshimiwa Spika, mradi umeshaanza kutekelezwa kwa maana ya kwamba tayari maeneo kama ya New Forest na Mchangani Mkandarasi ameshaanza kujenga camp ili kuona kwamba anafanya mobilization lakini maeneo ya Intake na maeneo ya Sistila kule juu karibu ya MUST wanaendelea na clearance kwa ajili hiyo ya kujenga camp kuona kwamba kazi zitaanza mara moja lakini suala lililoko mezani kwa sasa hivi, tayari Wizara ya Fedha imetoa exchequer ambayo imeingia kwenye Wizara ya Maji ukiisoma unaiona sasa hivi tunachosubiri tu ni fedha kuingia kwenye account na mamlaka kuweza kuingiziwa hiyo fedha mara moja Mkandarasi alipwe aendelee na mradi. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa hiyo hela zinachelewa wapi kwenu au Wizara ya Fedha?

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, Wizara ya Fedha.