Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 44 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 576 2023-06-09

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI K.n.y. MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza:-

Je, lini Mifumo ya Malipo ya Kimataifa itaruhusiwa ili wabunifu/watu wanaofanya kazi za ushauri kwa taasisi za nje wapate malipo?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante na kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Faustine Ndugulile, Mbunge wa Kigamboni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Mifumo ya Malipo ya Taifa ya mwaka 2015 inawataka watoa huduma za mifumo ya malipo kupata leseni kutoka Benki Kuu ya Tanzania ili kutoa huduma hizo nchini. Utaratibu huu unaiwezesha Benki Kuu kuwa na usimamizi wa moja kwa moja kwa watoa huduma za mifumo ya malipo nchini na kuhakikisha panakuwa na mifumo ya malipo inayoaminika na salama kwa wananchi wetu.

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia sheria hiyo, Benki Kuu imeweza kutoa leseni kwa watoa huduma za mifumo ya malipo wa kimataifa ambapo wamefungua ofisi zao nchini, ambapo hadi Aprili mwaka 2023 jumla ya taasisi 10 za kimataifa ambazo si benki za biashara zimepewa leseni ya kutoa huduma za mifumo ya malipo nchini.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuhakikisha kuwa leseni za kutoa huduma za mifumo ya malipo zinatolewa kwa watoa huduma wote, wa ndani na nje ya nchi, waliotayari na wanaokidhi matakwa ya sheria ili kutoa fursa kwa wananchi kupata huduma stahiki za mifumo ya malipo zinazozingatia usalama wa fedha zao na maslahi mapana ya nchi. Ahsante.