Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 44 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 577 2023-06-09

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Arusha – Mirongoine – Simanjiro – Terati hadi Kongwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Noah Lemburis Saputu Mollel, Mbunge wa Arumeru Magharibi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara ya Arusha – Mirongoine – Simanjiro – Kongwa inajulikana kwa jina la Arusha – Kibaya – Kongwa yenye urefu wa kilometa 453. Serikali itajenga barabara hii kwa kiwango cha lami kwa utaratibu wa Engineering, Procurement, Construction plus Finance (EPC + F). Hadi sasa Mkandarasi amekwishapatikana na mkataba wa ujenzi utasainiwa kabla ya mwisho wa mwezi Juni, 2023. Ahsante.