Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Arusha – Mirongoine – Simanjiro – Terati hadi Kongwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Spika, ni lini mtapandisha hadhi barabara ya Uchira – Kisomachi - Kolarie?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge, kuhusu kupandisha hadhi hizi Barabara, kuna taratibu zake, ambapo kama Mheshimiwa Mbunge pamoja na vikao vya kuanzia wilaya, mkoa wataleta maombi, Wizara ya Ujenzi ambayo watakwenda kufanya tathmini na baada ya hapo kama itakidhi vigezo, maana yake ni kwamba hiyo barabara itakuwa imepandishwa hadhi. Pia kama itakuwa barabara hiyo haikupandishwa hadhi, wanaweza kuomba kukasimiwa kukarabatiwa ama kusimamiwa na TANROADS, ahsante.

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Arusha – Mirongoine – Simanjiro – Terati hadi Kongwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Barabara ya Kigamboni mpaka Kongowe eneo la Mikwambe lina tatizo ya mifereji: Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga mifereji katika barabara hiyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja, siyo tu mifereji, bali pia ni barabara ambayo kuna vipande vingi ambavyo vimechoka sana. Kwa hiyo, mpango wa Serikali pamoja na kutengeneza mifereji, pia ni kukarabati yale maeneo yote ambayo yamechakaa sana, ahsante.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Arusha – Mirongoine – Simanjiro – Terati hadi Kongwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hiyo. Barabara ya Kolandoto kwenda Kishapu ina kero kubwa kwa wasafiri na wasafirishaji. Ni lini Serikali itaanza kutekeleza mradi huu katika kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ya Kolandoto - Kishapu – Lalago, ni moja ya barabara kuu na Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba katika mpango huu wa fedha kwa maana ya bajeti ambayo tumepitishiwa, tayari tumeshatenga fedha kwa ajili ya kuanza kuijenga barabara hiyo kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Norah Waziri Mzeru

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Arusha – Mirongoine – Simanjiro – Terati hadi Kongwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. NORAH W. MZERU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii; je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati barabara ya kutoka Nanenane – Tungi kupita VETA kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tumekuwa na utaratibu wa kufanya matengenezo ya barabara zote kwa kiwango cha lami, kwa hiyo hata mwaka unaokuja wa fedha tumetenga kwa ajili ya kukarabati maeneo yote ambayo yameharibika ili kuhakikisha kwamba barabara inarudi kwenye ubora wake. Ahsante.


Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Arusha – Mirongoine – Simanjiro – Terati hadi Kongwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Kuna changamoto kubwa sana ya mlundikano wa malori ndani ya Mji wa Tunduma ambao unasinyaza na kufubaza uchumi wa Wana-Tunduma. Serikali mna mpango gani wa kujenga njia ya dharura ili kunusuru hali iliyopo kwenye Mji wa Tunduma? Nashukuru sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Stella Fiyao, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kwamba kuna msongamano mkubwa sana katika Mji wa Tunduma ambao ndipo tunapotoka pale kwenda Zambia. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Tunduma kwamba tunakwenda siyo tu kufanya mpango wa dharura, lakini mpango kamili wa kujenga barabara ya njia nne katika Mji wa Tunduma ambapo tutakwenda kujenga kwa mpango wa EPC+F.

Mheshimiwa Spika, moja ya maeneo ambayo tunategemea kuanza ni pamoja na miji ya Tunduma ili kukwamua na kuondoa changamoto ambayo ipo inayosababisha msongamano mkubwa katika Mji wa Tunduma. Kwa hiyo, mkataba huo tunategemea utasainiwa Juni mwaka huu wa fedha, ahsante. (Makofi)

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Arusha – Mirongoine – Simanjiro – Terati hadi Kongwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 6

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Makanya – Ruvu ambayo inakwenda kwenye machimbo ya gypsum? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ni barabara ya kimkakati ambayo inaenda kwenye maeneo muhimu ya kiuchumi. Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuijenga hiyo barabara kwa kiwango cha lami.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Arusha – Mirongoine – Simanjiro – Terati hadi Kongwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 7

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Ningependa kujua ni lini barabara ya kiusalama kutoka Susuni – Mwema - Sirari – Mriba – Nyamongo itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami mara tu tutakapokuwa tumekamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina.

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Arusha – Mirongoine – Simanjiro – Terati hadi Kongwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 8

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Kwa kuwa, barabara hii inahudumia mikoa mitatu Arusha, Manyara na Dodoma. Je, Serikali haioni sasa ni muhimu kuharakisha barabara hii ili kujenga uchumi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Je, kwa kuwa barabara hii iko kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya 2020/2025, Serikali haioni kutoharakisha barabara hii ni kutotekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya 2020/2025? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili kwa pamoja ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika jibu la msingi, ni kweli barabara hii iko kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi lakini pia ni kweli inaunganisha Mikoa mitatu, kwa maana hiyo ndiyo maana katika jibu langu la msingi hii barabara imetengewa fedha na tumeipitisha inaanza kujengwa kwa EPC+F na kama nilivyosema tutaisaini kuanza ujenzi wa barabara hii kabla ya mwisho wa mwaka wa fedha kwa mwaka huu, kwa maana ya huu mwezi Juni. Ahsante. (Makofi)

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Arusha – Mirongoine – Simanjiro – Terati hadi Kongwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 9

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Je, Serikali haioni kwamba ni busara kukamilisha barabara ya Kilosa kwenda Mikumi ili kuongeza tija kwenye uwekezaji mkubwa wa reli ya SGR pale Kilosa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge wa Mikumi, siyo tu busara, lakini kwa kweli ni barabara ambayo ni muhimu, ambayo sasa itakuwa inaunganisha barabara ambayo tunaijenga kwa EPC kuanzia Namtumbo – Malinyi – Mikumi ambayo tunaona busara badala mtu kwenda Morogoro, itoke Mikumi kuja Kilosa. Kwa hiyo, hiyo mipango ipo kuhakikisha kwamba tunapafungua kati ya Kilosa na kuunganisha na Mikumi, ahsante.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Arusha – Mirongoine – Simanjiro – Terati hadi Kongwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 10

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara inayoanzia Nanganga kwenda Ruangwa inajengwa sasa kwa kiwango cha lami. Hata hivyo, wakazi wa Nanganga wanadai fidia. Ni lini Serikali italipa fidia kwa watu waliobomolewa nyumba zao eneo la Nanganga? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:_

Mheshimiwa Spika, tumekuwa na utaratibu wa kulipa fidia tunapoanza ujenzi wa barabara zote. Namwomba Mheshimiwa Mbunge, kama kuna changamoto kwa hiyo barabara, tuweze kuonana ili tujue tatizo ni nini ambapo wananchi hao wanaodai mpaka sasa hivi wakati barabara inajengwa na tulitatue kwa kuwalipa fidia hao wananchi wa barabara ya Nanganga hadi Ruangwa, ahsante.

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Arusha – Mirongoine – Simanjiro – Terati hadi Kongwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 11

MHE. ENG. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Je, Serikali imefikia hatua gani katika maandalizi ya kuijenga barabara ya Haydom -Mogitu kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, barabara ya Mogitu - Haydom ni barabara ambayo ni link kwenye ile barabara ya Karatu - Mbulu – Haydom kwenda Lalago. Kwa hiyo, ni link ya hiyo barabara. Kwa hiyo, ni sehemu ya hiyo barabara, ahsante.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Arusha – Mirongoine – Simanjiro – Terati hadi Kongwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 12

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Ni lini Serikali itatimiza ahadi yake ya kujenga kilometa kumi za lami kwenye mitaa ya Mji wa Bunda?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, kwa kushirikiana na wenzetu wa TAMISEMI, ipo mipango ya kutimiza hiyo ahadi ya kujenga barabara ya kilometa kumi ambazo ziliahidiwa na viongozi wetu katika Mji wa Bunda kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Arusha – Mirongoine – Simanjiro – Terati hadi Kongwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 13

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Mbuguni kwa kiwango cha lami ambayo inaanzia Tengeru hadi Mererani?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Barabara aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge, ni ya kimkakati ambayo inakwenda machimbo ya Tanzanite. Mheshimiwa Mbunge atakuwa shahidi kwamba mpaka sasa hivi tunaendelea kukamilisha usanifu wa kina na baada ya hapo Serikali itatafuta fedha kwa ajili ya kuijenga sasa kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Barabara ya Arusha – Mirongoine – Simanjiro – Terati hadi Kongwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 14

MHE. ASKF. JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Spika, ni ahadi ya Mheshimiwa Rais kwamba barabara ya kutoka Bunju B mpaka Mabwepande ijengwe kwa kiwango cha lami katika Jimbo la Kawe: Ni lini Serikali itatimiza ahadi hiyo?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Kawe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ya Bunju B – Mabwepande – Magohe – Mapigi hadi Kibamba, ni moja ya barabara ambayo sasa hivi inafanyiwa usanifu. Siyo tu ahadi ya viongozi, lakini tunategemea ndiyo itakuwa altering ya barabara za Mji wa Dar es Salaam. Kwa hiyo, ipo kwenye mpango na tunavyoongea sasa hivi Washauri Wahandisi wako kazini wanafanya usanifu, ahsante.