Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 46 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 584 2023-06-12

Name

Asya Sharif Omar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARYAM AZAN MWINYI K.n.y. MHE. ASYA SHARIF OMAR aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa huduma ya kifungua kinywa kwa wanafunzi wa shule za msingi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Asya Sharif Omar, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inatambua umuhimu wa upatikanaji wa huduma ya chakula kwa wanafunzi wanapokuwa shuleni wakati wa masomo katika kupunguza utoro, kuongeza usikivu na kuboresha afya.

Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia umuhimu huo, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imetoa Mwongozo wa Kitaifa wa Huduma ya Chakula na Lishe kwa wanafunzi Elimumsingi unaoelezea taratibu za mifumo ya uchangiaji wa huduma ya chakula shuleni. Aidha, Serikali iliwaelekeza Viongozi wa Mikoa na Halmashauri kusimamia mwongozo wa Lishe wa Mwaka 2021.

Mheshimiwa Spika, nichukue fursa hii, kuwaomba Waheshimiwa Wabunge kushirikiana na viongozi wa Mikoa na Mamlaka ya Serikali za Mitaa ili kuona namna bora ya utekelezaji wa mwongozo wa lishe na kuwawezesha wanafunzi kupata chakula shuleni.