Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 46 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 589 2023-06-12

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PROF. SHUKRANI E. MANYA K.n.y. MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza:-

Je, lini Serikali itapeleka vifaa kwenye Jengo Jipya la Mama na Mtoto katika Hospitali ya META Mkoani Mbeya?

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Afya, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Suma Ikenda Fyandomo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetoa fedha kiasi cha shilingi bilioni 5.4 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa na vifaatiba kwa ajili ya jengo la huduma za Mama na Mtoto katika Hospitali ya Meta, Mkoa wa Mbeya. Aidha, vifaatiba hivyo vimeshaanza kupelekwa na kufungwa katika jengo la Mama na Mtoto kupitia Bohari Dawa (MSD).

Mheshimiwa Naibu Spika, jengo hili limeanza kutumika na ufungaji wa vifaatiba katika vitengo mbalimbali unaendelea na utakamilika mapema mwezi Julai, 2023. Naomba kuwasilisha.