Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 46 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 591 2023-06-12

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza:-

Je, lini Serikali itaanza ukarabati mkubwa wa barabara kuu ya Makambako - Njombe?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deodatus Philip Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ina mpango wa kuifanyia ukarabati barabara yote ya kutoka Makambako – Njombe – Songea yenye urefu wa kilometa 295. Sehemu ya Lutukila – Songea kilometa 95 ipo katika mpango wa ukarabati kupitia Mradi wa Tanzania Transport Integrated Project (TANTIP) ambapo Mkataba wa Mkopo nafuu kati ya Serikali na Benki ya Dunia umesainiwa na zabuni za kumpata Mkandarasi wa ujenzi zinatarajiwa kutangazwa mwezi Juni, 2023.

Mheshimiwa Naibu Spika, sehemu iliyobaki ya Lutukila – Makambako ikiwemo na sehemu ya Makambako – Njombe urefu wa kilometa 59, Serikali inaendelea kutafuta fedha toka vyanzo mbalimbali vya ndani na nje kwa ajili ya ukarabati. Ahsante.