Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deodatus Philip Mwanyika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ukarabati mkubwa wa barabara kuu ya Makambako - Njombe?

Supplementary Question 1

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya Serikali. Napenda kusema tunashukuru sana Serikali hata kwa hicho cha kuanza na ukarabati wa barabara kutoka Songea mpaka Lutukila. Hata hivyo ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza, barabara hii ni mbaya sana, ni barabara kubwa ya kiuchumi na kuna shughuli nyingi sana sasa hivi. Sasa Serikali, wakati fedha zinatafutwa, hawaoni kwamba kuna umuhimu wa angalau kutenga fedha za kutosha ili maeneo ambayo ni hatarishi kwa magari mengi ya mkaa yaweze kuanza kushughulikiwa kwenye kona kali na miteremko?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Barabara hii ilifanyiwa redesign 2012, wakati huo Njombe haikuwa mkoa. Mji wa Njombe ambapo barabara hiyo inapita umebadilika, unakua kwa kasi, umekuwa na activities nyingi. Sasa Mheshimiwa Naibu Waziri anaweza kutoa maelekezo kwamba sasa wafanye redesign pale katikati ya mji kutoka Kibena mpaka kufika Nundu ili paendane na uhalisia wa Mji wa Njombe ambao unaenda kuwa Manispaa? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Deodatus Phillip Mwanyika, Mbunge wa Njombe Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni utaratibu ambao umezoeleka kwamba katika hizi barabara kubwa, na hasa barabara aliyoitaja ni ya zamani, tumeendelea na tutaendelea kutenga fedha kwa ajili ya kufanya ukarabati maeneo yale yote ambayo yanakuwa yamechakaa sana ili kuhakikisha kwamba wanaosafiri na wasafirishaji hawapati changamoto. Kwa hiyo, nimtoe wasiwasi huo Mheshimiwa Mbunge, Serikali itaendelea kukarabati yale maeneo yote korofi katika hiyo barabara.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili, ni kweli kama alivyosema, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Njombe ni mji unaokua sana kama mji na unapitisha magari mengi makubwa. Sisi kama Wizara tunataka tumhakikishie kwamba tutafanya redesign. Itakuwa ni dual carriageway katika Mji wa Njombe kuanzia Kibena Hospitali hadi Hagafilo na zitakuwa ni njia nne ili kuhakikisha kwamba hakutokei changamoto ya msongamano katika Mji wa Njombe, ahsante. (Makofi)

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. DEODATUS P. MWANYIKA aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ukarabati mkubwa wa barabara kuu ya Makambako - Njombe?

Supplementary Question 2

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kufahamu Serikali imefikia hatua gani katika maandalizi ya kuijenga barabara ya Kondoa – Gisambalang – Nangwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Barabara ambayo ameitaja kwa kweli mpango mkubwa hasa ni kuhakikisha kwamba kuna daraja kubwa ambalo linaleta changamoto kati ya Kondoa na Hanang. Tunachofanya sasa hivi, kwanza ni kufanya usanifu wa lile daraja, tulijenge, halafu tuimarishe hiyo barabara ili iweze kupitika kipindi chote cha mwaka. Sasa hivi kwa kweli inapotokea masika hiyo barabara haipitiki, ahsante.