Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 46 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 592 2023-06-12

Name

Taska Restituta Mbogo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TASKA R. MBOGO aliuliza: -

Je, lini Serikali itakamilisha ujenzi wa meli tatu kwa ajili ya Ziwa Tanganyika kama ilivyoahidi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Taska Restituta Mbogo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali kupitia Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) imetenga bajeti katika mwaka wa fedha 2022/2023 kwa ajili ya kutekeleza miradi ya ujenzi wa meli mpya mbili; meli moja ya kubeba mizigo tani 3,500 na meli moja ya kubeba abiria 600 na mizigo tani 400 katika Ziwa Tanganyika. Kwa sasa MSCL ipo katika hatua za mwisho za majadiliano na mkandarasi ili kuwezesha kuanza ujenzi wa meli hizo. Mikataba ya ujenzi wa meli hizo inatarajiwa kusainiwa mwishoni mwa Juni, 2023.

Mheshimiwa Naibu Spika, aidha, jitihada zinafanywa na Serikali za kukarabati Meli ya MV Liemba. Kwa sasa Serikali ipo katika hatua za mwisho za majadiliano na mkandarasi kabla ya mkataba wa ukarabati wa Meli ya MV Liemba kusainiwa, ahsante.