Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 46 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 594 2023-06-12

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA K.n.y. MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: -

Je, kuna mpango gani kuboresha utendaji wa Shirika la Mbolea (TFC) ili kusambaza pembejeo kwa wakulima kwa wakati?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Josephat Sinkamba Kandege, Mbunge wa Kalambo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika msimu wa mwaka 2022/2023 Serikali imeunda Bodi ya Wakurugenzi na kuajiri Meneja Mkuu wa Kampuni ya Mbolea Tanzania. Vilevile, Serikali imeipatia TFC mtaji wa Shilingi bilioni sita ambao umeiwezesha kununua jumla ya tani 4,500 na kusambaza jumla ya tani 3,851.35 za mbolea kwa wakulima 20,271.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2023/2024, Serikali imepanga kuiongezea TFC mtaji wa Shilingi bilioni 40 kwa ajili ya kununua na kusambaza pembejeo za kilimo kwa wakulima. Aidha, mpango wa muda mrefu ni kampuni kujenga kiwanda cha kuchanganyia mbolea na eneo la ekari 14.5 limepatikana kwenye Kijiji cha Visegese, Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe, Mkoa wa Pwani, ambapo ujenzi utaanza katika mwaka wa fedha wa 2023/2024.