Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jonas William Mbunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA K.n.y. MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: - Je, kuna mpango gani kuboresha utendaji wa Shirika la Mbolea (TFC) ili kusambaza pembejeo kwa wakulima kwa wakati?

Supplementary Question 1

MHE. JONAS W. MBUNDA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Pia naomba niipongeze Serikali kwa kuchukua jitihada kuhakikisha kwamba shirika hili linafanya kazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa shirika hili muda mrefu halijafanya kazi, ni wazi kwamba kuna upungufu mkubwa sana wa wafanyakazi. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba inaongeza wafanyakazi katika shirika hilo?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Kama nilivyosema awali kwamba ni muda mrefu TFC haijafanya kazi, ni obvious kwamba miundombinu ya maghala ambayo yalikuwa yanatumika kuhifadhia mbolea yana hali mbaya: Serikali imeandaa mpango gani kuhakikisha kwamba maghala haya yanakarabatiwa? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la wafanyakazi, ni kweli kampuni hii inahitaji wafanyakazi. Wiki iliyopita, management yote ilikuwa hapa kwa ajili ya kwenda kuutetea muundo kwa ajili ya kuanza kuboresha eneo hili na kupata wafanyakazi wapya. Nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba kazi hii inaendelea ya kupata wafanyakazi wengine wa kusaidia kuendesha Kampuni yetu ya TFC.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili kuhusu maghala, ni kweli tunayo maghala ambayo yamekuwa na changamoto kwa kiwango kikubwa sana, lakini hivi sasa tunashirikiana na Halmashauri za wilaya husika kwa ajili ya maghala yale ambayo yapo katika maeneo yao tuweze kuyatumia. Pia sisi tunayo maghala yetu ambayo tunayaboresha hivi sasa ili yaanze kufanya kazi hii. Katika fedha ambayo tumeipanga mwaka ujao wa bajeti, pia tumeongeza eneo la kuboresha maghala yetu ili yaweze kutumika vizuri.

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA K.n.y. MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: - Je, kuna mpango gani kuboresha utendaji wa Shirika la Mbolea (TFC) ili kusambaza pembejeo kwa wakulima kwa wakati?

Supplementary Question 2

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Kampuni yetu ya Mbolea ilikopesha wananchi, watu binafsi, vyama vya ushirika na Serikali zaidi ya Shilingi bilioni 18 ambayo ilisababisha kampuni ikawa na mtaji hasi: Je, Serikali ina mpango gani wa kukusanya haya madeni ili kuiongezea nguvu Kampuni yetu ya Mbolea?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, suala la madeni ni kweli na moja kati ya kazi ambazo tumeipa management hivi sasa ni kuhakikisha inafuatilia madeni yote na kuhakikisha kwamba madeni haya yanalipwa ili kuongeza mtaji wa Kampuni ya TFC.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. JONAS W. MBUNDA K.n.y. MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE aliuliza: - Je, kuna mpango gani kuboresha utendaji wa Shirika la Mbolea (TFC) ili kusambaza pembejeo kwa wakulima kwa wakati?

Supplementary Question 3

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Msimu uliopita wananchi wa Wilaya ya Tarime walipata shida sana kupata mbolea. Walikaa mpaka wiki tatu pale Tarime waking’ang’ania mbolea: Naomba nipate kauli ya Serikali kwamba msimu ujao wa kilimo watu wa Tarime watapata ile shida au itakuwa imeisha? Ahsante. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli katika msimu uliopita tulikuwa tuna changamoto ya upatikanaji wa mbolea kwa wakati, lakini Serikali imechukua hatua. Tumeshamwelekeza Mkurugenzi Mtendaji wa TFRA na timu yake nzima kuhakikisha kwamba wanaongeza vituo vya mawakala wa uuzaji wa mbolea sambamba na kutumia vyama vya ushirika kama sehemu ya usambazaji wa mbolea.

Mheshimiwa Naibu Spika, kubwa kuliko yote, nataka niwaondoe hofu Waheshimiwa Wabunge kwamba mbolea itaanza kuingia nchini mapema mwezi Julai ili wakulima waanze kuinunua mapema kujiandaa na msimu unaokuja.