Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 46 Water and Irrigation Wizara ya Maji 596 2023-06-12

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza: -

Je, ni lini Mkandarasi wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria kwenye Vijiji 33 vya Jimbo la Bunda ataanza kazi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Boniface Mwita Getere, Mbunge wa Jimbo la Bunda kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeajiri Mtaalam Mshauri kwa ajili ya kufanya usanifu wa mradi wa kutoa maji Ziwa Victoria kwenda vijiji 33 vya Wilaya ya Bunda utakaokamilika mwezi Julai, 2023. Vilevile, Mtaalam Mshauri huyo ataandaa pia makabrasha ya zabuni kwa ajili ya kuajiri mkandarasi wa ujenzi atakayeanza kazi katika mwaka wa fedha 2023/2024. Aidha, katika kupunguza adha ya maji kwa wananchi wa Wilaya ya Bunda wakati wakisubiri mradi mkubwa, katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali inaendelea kuboresha huduma ya maji Wilayani Bunda kwa kujenga miradi ya maji ya Kiroleri-Kambubu, Mariwanda na Hunyari. Miradi hiyo inatarajia kukamilika mwezi Julai, 2023.