Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza: - Je, ni lini Mkandarasi wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria kwenye Vijiji 33 vya Jimbo la Bunda ataanza kazi?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na ninashukuru kwa majibu ya Serikali. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa sasa Serikali imetamka wazi kwamba mradi huu utaanza bajeti ijayo 2023/2024 sasa Serikali inaweza kuwaambia wananchi wa Bunda kwamba ni Bajeti kiasi gani imetengwa kwa mradi huo?

Swali la pili; kwa kuwa Serikali imetumia zaidi ya milioni 52 kufanya usanifu yakinifu kama kuchimba malambo ya Salama A, Lakana, Burundu, Kambugu, Tingirima na Mihingo. Je, ni lini miradi hii itakamilika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Boniphace Getere kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na bajeti kwenye Jimbo la Bunda, Mheshimiwa Mbunge unafahamu na nikupongeze kwanza kwa ushirikiano wako ulifika Wizarani umeweza kukutana na Waziri na Katibu Mkuu. Yote hii ni jitihada ya kuona kwamba hili linafanyika. Kwa eneo lako la Bunda zaidi ya bilioni 1.7 imepangwa na itaenda kutumika kutokana na zile bilioni 750 kwenye ule mradi wa Ziwa Victoria kwako ni zaidi ya bilioni 1.7.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na uchimbaji na ukamilishaji wa haya mabwawa Mheshimiwa Mbunge, Mheshimiwa Waziri alishakuelekeza vizuri na tumshukuru zaidi Mheshimiwa Rais kwa kutupatia sisi Wizara ya Maji vifaa au vitendea kazi. Tumeshapata mitambo na huu mtambo mmojawapo wa kuchimba mabwawa unaletwa Bunda mahsusi kuhakikisha haya Mabwawa yanakwenda kuchimbwa na yanakamilika na Mheshimiwa Mbunge tutakuharifu tutakwenda pamoja kwa sababu tunashirikiana vizuri.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza: - Je, ni lini Mkandarasi wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria kwenye Vijiji 33 vya Jimbo la Bunda ataanza kazi?

Supplementary Question 2

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa tayari Mkandarasi anayetekeleza mradi wa Nduku Busangi Ntobo na mradi wa Mwarugulu tayari amesha supply vifaa na hajalipwa fedha. Kufanya hivyo, umesababisha mradi kusimama. Ni lini sasa Wizara itaenda kumlipa fedha mkandarasi ili aweze kutekeleza miradi hiyo miwili ya Mwarugulu na mradi wa Busangi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi hii yote uliyoitaja ni kweli utekelezaji unaendelea na ulipwaji wa madeni kwa wakandarasi tayari tumeanza kama Wizara. Fedha tunavyozipata tunaendelea kupunguza madeni na kuhakikisha wakandarasi wote walipwe ili waweze kuendelea na miradi hii.