Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 46 Water and Irrigation Wizara ya Maji 597 2023-06-12

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itachimba visima katika Shule ya Sekondari Ndono Uyui?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Athuman Almas Maige, Mbunge wa Jimbo la Tabora Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, nia ya Serikali ni kuona maji yanapatikana kwa ajili ya matumizi ya jamii, maendeleo ya kiuchumi na mazingira. Shule ya Sekondari Ndono ilikuwa na changamoto ya maji, na katika mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imepeleka maji shuleni hapo kupitia kisima kilichopo katika Zahanati ya Kijiji cha Ndono na sasa wanafunzi wanapata maji safi na salama. Aidha, Serikali imeanza maandalizi ya utekelezaji wa mradi wa upanuzi wa bomba la maji kutoka mradi wa Ziwa Victoria kwenda Wilaya za Urambo na Kaliua ambapo wananchi wa Kijiji cha Ndono ikiwemo wanafunzi wa shule ya Sekondari ya Ndono wataongezewa upatijanaji wa huduma ya maji.