Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itachimba visima katika Shule ya Sekondari Ndono Uyui?

Supplementary Question 1

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, haya ndio majibu bora kabisa ya Serikali, natoa pongezi kwa Mama Samia Suluhu Hassan lakini pia Waziri Aweso na Waziri Prisca Mahundi. Niliomba maji haya kwa ajili ya shule hiyo na nimepewa na wanafunzi pale na jamii yote niipongeze Serikali sana sana, naomba nitoe shukrani zangu.

Mheshimiwa Naibu Spika, nina swali moja tu la nyongeza. Shule hii ina wanafunzi 1500 na ni wengi sana kwa hiyo bill ya maji, ankara imekuwa kubwa sana. Je, Serikali inaweza kutoa ruzuku sehemu ya ankara hii ili wote wapate maji, sasa wanafunzi wanachangia maji?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Awali ya yote nipende kupokea pongezi za Mheshimiwa Mbunge lakini na yeye pia ni kupitia jitihada zake kama mwenyewe anavyosema, alikuja ofsini tuliweza kuongea kwa pamoja na maombi yake tumeyafanyia kazi. Kuhusiana na kuona mradi huu unabaki kuwa endelevu suala la bill shuleni na wanafunzi wote waweze kupata maji kila siku, Mheshimiwa Mbunge nimelipokea tutalifanyia kazi kwa pamoja.

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itachimba visima katika Shule ya Sekondari Ndono Uyui?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kupata nafasi. Mtaa wa Mikwambe Kata ya Twaangoma kuna mgogoro wa kisima cha maji ambacho kimejengwa katika kiwanja ambacho amemilikishwa mtu binafsi. Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua mgogoro huo ili wananchi waendelee kupata maji safi na salama?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Chaurembo kama ifauatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli mgogoro huo upo lakini DAWASA tayari wanaufanyia kazi na kwa niaba ya Wizara DAWASA watahakikisha mgogoro huu unaisha kwasababu maeneo ya aina hii yamekuwa mengi na tumekuwa tukimaliza. Kwa hiyo, hata hili pia sisi kama Wizara tutahakikisha linakamilika ili huu mradi uweze kutoa huduma kwa wananchi.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itachimba visima katika Shule ya Sekondari Ndono Uyui?

Supplementary Question 3

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kumekuwa na changamoto ya wanafunzi kwenye Jimbo la Momba kupoteza maisha kwa ajili ya kwenda kufata maji mtoni. Siku za usoni tulipoteza mwanafunzi wa Momba Secondary na tukapoteza mwanafunzi wa Sekondari ya Kamsamba kwa sababu wanaenda kufata maji mtoni kwa mwendo mrefu. Je, ni ipi kauli ya Wizara ya Maji kwa udharula wake kwenda kutuchimbia visima kwenye hizi Sekondari ili tusiendelee kupoteza maisha ya watoto wetu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Condester kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikupe pole sana kwa wananchi kupata kadhia hizi lakini sisi kama Wizara ni sehemu ya kuona kwamba tunafikisha maji safi na salama maeneo yote yanayotoa huduma, na kwa eneo hili la shule naomba nikuahidi kwamba tutakuja kuwachimbia kisima na kama kuna kisima jirani basi tutafanya extension ili kuhakikisha wanafunzi hawaendi mtoni na kupata madhara.