Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 46 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 598 2023-06-12

Name

Maimuna Ahmad Pathan

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA A. PATHAN aliuliza:-

Je, ni lini tatizo la kukatika umeme mara kwa mara Mkoani Lindi litakwisha?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna Ahmad Pathan, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Lindi unapata umeme kutoka katika vyanzo viwili ambavyo ni mitambo ya kufua umeme wa gesi iliyopo Mtwara na Lindi (Somanga).

Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi kifupi (siku 90), Serikali imeandaa mkakati wa kuongeza upatikanaji wa umeme mikoa ya Lindi na Mtwara kwa kupeleka jenereta ya megawati 20, kufanya ukarabati wa miundombinu ya kusambaza umeme na kufunga vifaa vinne vya kuzima na kuwasha umeme (Autoclosers) kwenye njia mchepuko. Utekelezaji wa Mipango hii ulianza mwezi Mei, 2023.

Mheshimiwa Naibu Spika, mikakati mitatu ya muda mrefu ni kujenga njia yenye msongo wa kilovoti 220 Songea – Tunduma (mradi huu ulianza mwezi Machi, 2023 na utachukua miezi 18). Kujenga njia yenye msongo wa kilovoti 220 Tunduru – Masasi, Mkandarasi atakabidhiwa eneo la mradi mwezi Juni, 2023. Ujenzi wa njia yenye msongo wa kilovoti 220 Masasi - Mahumbika ambayo upembuzi utaanza mwaka wa fedha 2023/2024.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika hatua nyingine kubwa, Serikali inaendelea na mazungumzo na Shirika la Maendeleo la Japan (JICA) juu ya ujenzi wa kituo kikubwa kitakachozalisha Megawati 300 Mkoani Mtwara.

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi hii itakapokamilika, hali ya umeme katika mikoa ya Mtwara na Lindi itaimarika sana.