Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 46 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 599 2023-06-12

Name

Naghenjwa Livingstone Kaboyoka

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NAGHENJWA L. KABOYOKA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itafanya tathmini ya kampuni zilizo chini ya NARCO ili kuona tija zake katika uchumi?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Naghenjwa Livingstone Kaboyoka, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) inamiliki ranchi 15 na imewekeza katika ranchi nane kati ya hizo. Aidha, NARCO imegawa vitalu na kukodishwa kwa wafugaji na kampuni binafsi kwa ajili ya ufugaji wa kisasa na wa kibiashara. Mwezi Oktoba, 2022 Serikali kupitia Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) ilifanya tathmini kwenye vitalu 116 ambavyo vimekodishwa kwa wafugaji ili kubaini hali ya uwekezaji kulingana na mipango ya biashara iliopo kwenye mikataba yao. Katika tathmini hiyo ilibainika kuwa wawekezaji 76 wamewekeza kulingana na mkataba na wawekezaji 40 wameonesha kutofanya vizuri kulingana na mikataba yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia tathimini ilibaini kuwa NARCO inakabiliwa na changamoto za kimtaji, hivyo imeandaa andiko la mabadiliko ili kuiwezesha kupata mtaji kutoka vyanzo mbalimbali vya fedha. Hata hivyo, ili kuimarisha Kampuni ya NARCO na kuongeza tija, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imewekeza kiasi cha shilingi bilioni 4.6 kwa ajili ya kununua ng’ombe wazazi, kuchimba visima virefu na kununua mitambo ya kulima, kuvuna na kuhifadhi malisho ya mifugo.