Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 47 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu 601 2023-06-13

Name

Bonnah Ladislaus Kamoli

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Segerea

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI K.n.y. MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza:-

Je, Serikali imejipangaje kushirikiana na Sekta Binafsi kuhakikisha vijana wanaohitimu wanapata ajira?

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bonnah Ladislaus Kamoli, Mbunge wa Segerea, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuhakikisha vijana wanaohitimu wanapata ajira, Serikali kwa kushirikiana na Sekta Binafsi imejipanga kufanya yafuatayo:-

(i) Kuendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji ili kuwezesha Sekta Binafsi kuwekeza kwenye sekta zinazoweza kuzalisha fursa nyingi za ajira na hivyo kuwezesha vijana wengi wahitimu kupata fursa za ajira;

(ii) Kuendelea kutekeleza programu ya mafunzo ya uzoefu wa kazi (Internship) kwa vijana wahitimu wa ngazi mbalimbali za elimu na mafunzo ili kuwawezesha vijana husika kuwa na ujuzi unaohitajika na waajiri wa Sekta Binafsi wa ndani na nje ya nchi;

(iii) Serikali inaendelea kufanya majadiliano na Nchi za kimkakati kwa lengo la kuwezesha kuwa na Hati za Mashirikiano ya Uwili (Bilateral Agreements) ili kuwezesha Watanzania kunufaika na fursa za ajira zinazotokana na utangamano wa kikanda pamoja na ushirikiano wa kidiplomasia;

(iv) Serikali kupitia Wizara ya Kilimo inaendelea kutekeleza Programu ya kuwezesha vijana kushiriki katika Kilimo Biashara (Building a Better Tomorrow Youth Initiative for Agribusiness – BBTYIA);

(v) Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi inaendelea kutekeleza programu ya mafunzo ya vitendo (Atamizi) kwa wahitimu wa fani za uvuvi na ukuzaji viumbe maji; na

(vi) Serikali kupitia Wizara ya Madini imeendelea kuwezesha wachimbaji wadogo wa madini kwa kuwatengea maeneo pamoja na kufanya utafiti ili kuwa na uhakika wa kupata madini, kuanzisha vituo zaidi ya 93 na Ofisi za masoko 42 za kuuzia madani na hii inawapa fursa za ajira, ahsante.