Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI K.n.y. MHE. BONNAH L. KAMOLI aliuliza:- Je, Serikali imejipangaje kushirikiana na Sekta Binafsi kuhakikisha vijana wanaohitimu wanapata ajira?

Supplementary Question 1

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; kwa kuwa Jiji la Dar es Salaam linauhitaji sana wa bidhaa za mbogamboga, je Serikali iko tayari kuwasaidia vijana wa Jimbo la Ilala kwa Mheshimiwa Bonnah kuwa na kitu kinaitwa urban farming na hivyo kuwawezesha kulima mazao ya mbogamboga ili kuliwezesha Jiji la Dar es Salaam kujitosheleza kwa bidhaa hiyo na wao kujipatia kipato?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa mazingira ya Dar es Salaam hayafanani sana na Jimbo la Mafinga Mjini. Je, Wizara na Serikali iko tayari kuwasaidia vijana wa Jimbo la Mafinga kuwapa mafunzo mahususi kwa ajili ya kutengeneza bidhaa za mazao ya misitu? (Makofi)

Name

Paschal Katambi Patrobas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shinyanga Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Bonnah Kamoli yaliyoulizwa na Mheshimiwa Cosato Chumi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, la kwanza, kama Serikali tuko tayari kuweza kuwasaidia vijana waweze kuona kwa kushirikiana na Halmashauri tutaangalia kama suala la urban farming linawezekana kulingana na upatikanaji wa eneo kwenye hilo eneo, lakini pia Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia maagizo ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ilishaagiza kila Halmashauri iweze kutenga maeneo kwa ajili ya vijana kufanya kilimo. Kwa hiyo tutaliangalia hilo na tunalizingatia ili kuweza kuhakikisha ombi hilo tunaenda kulitekeleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, lakini kabla ya hilo kuna program pia ya Vitalu Nyumba ambayo tumekuwa tukiitekeleza katika Halmashauri zote nchini zaidi ya 180. Tutaangalia na kuweza kuhakiki kama lot ya pili pia tutazidi kwenda kutoa vifaa na mafunzo ili waweze kunufaika.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili ambalo ameliuliza Mheshimiwa Mbunge kuhusiana na Mafinga. Kwa sura ileile hili tumelichukua na tutalizingatia, tutashirikiana na Mheshimiwa Mbunge ili tuweze kuona tunatengeneza mazingira mazuri ya vijana wetu kupata ajira,, ahsante.